Kabla ya kuanza kufanya marketing jiulize maswali yafuatayo


Marketing kwa maana moja mimi huwa naiita ni zao la Branding kwenye biashara ambalo linatakiwa litoke liende kuitangaza brand iliyojitengeneza.Hapa nchini biashara nyingi zinafanyika kwa mazoea na watu wanafanya bila kuelewa au kuwa na maana halisi ya kitu wanachokifanya, utakuta mtu ameona kampuni fulani wamefanya kitu fulani kwa ajili ya bidhaa, biashara au huduma kwa ajili ya kampuni yao, basi na yeye pia atataka kubadilisha jina tu kwenye hicho kitu kutoka jina  la biashara alioiona hadi jina la biashara yake, ila vingine ataviaacha kama vya mwenzake kwa vile tu amependa jinsi kile kitu kilivyo. Na wengine hufanya hivyo kwa mifano na kujaribu .

Leo nitaelezea kidogo vitu vya kuzingatia kabla hujaanza kujitangaza au kufanya marketing,Tutaangalia vitu kama vitano(5) ambavyo unatakiwa kuviangalia kwenye biashara yako kabla ya kuanza kufanya marketing, vitu hivi mara zote huwa ni vitu vya kawaida na huonekana ni sio vya muhimu sana lakini nikupe siri ndugu yangu hakuna kitu ambacho sio cha muhimu hata kama ni kidogo kiasi gani.

  1. Uko kwenye biashara gani?
Kabla ya kufanya marketing  lazima utambue uko katika biashara ya aina gani, kuna biashara za aina mbili huduma na bidhaa.Njia zake za kufanya marketing  (kutafuta masoko) zinatofautiana japo soko ni moja, kila biashara huwa inamtafuta mteja, mfano wa biashara zinazotoa huduma ni kama Washauri, Mahospitalini, n.k  na biashara zinatoa bidhaa ni kama Makampuni ya vinywaji, Maduka  n.k . Hivyo hata katika mbinu za utafutaji wake wa masoko zinakuwa tofauti, mbali na kutambua aina ya biashara ni lazima hapo hapo utambue na njia zake za kuingiza na kutoa pesa

  1. Malengo yangu ni yapi?
Baada ya kutambua aina yako ya biashara sasa unakuja hatua ya pili ambayo ni kutambua malengo, katika biashara malengo ni kitu cha muhimu na asilimia kubwa ya biashara zinazofanikiwa ni kwa sababu zimesimamia malengo na kuhakikisha yanafikiwa. Hivyo ni lazima biashara iwe na malengo na sio kampuni peke yake bali kila kinachofanyika ndani na nje ya biashara ni lazima kiwe na lengo ama malengo ambayo hayatakiwi kuwa na mwisho unaotofautiana.

  1. Nnatoa faida gani?
Faida pia ni kitu kingine kikubwa ambacho kinaongozwa na marketing na mauzo hivyo kabla ya kuingia katika kutafuta masoko inabidi kwanza utambue unatoa faida gani kwa biashara unayoifanya na unataka ikupe matokeo gani? na wewe mwenyewe na biashara mnatoa faida gani kwa mtumiaji wa mwisho na iwapo wewe ndio ungekuwa mtumija wa mwisho ungependa bidhaa au huduma itoleweje?.

         4 .  Nini ni faida nilizonazo kwenye ushindani?
Kabla ya kuingia katika ushindani sokoni ni lazima pia uangalie faida za ushindani, ambapo faida za ushindani ni kwako ni udhaifu wa mshindani ,sio tu kuanzisha kampeni kwa vile mwenzako ametengeneza kitu kama kile na wewe ufanye kwa kutegemea matokeo sawia, angalia kwanza unafaida gani za kiushindani na unazitumia vipi hapo ndio unaweza kufanya kitu ili kikuletee matokeo chanya.

           5.   Nnaogopa nini?
Kama mfanyabiashara au biashara lazima kuna vitu ambavyo utakuwa unaviogopa kwenye soko haijalishi vinaathari kwako au kwenye biashara, vitu hivyo pia vinatakiwa viwekwe hadharani kwa kuzingatia aina ya biashara na kampeni ya masoko unayotaka kuifanya hii itakusaidia kutengeneza njia nzuri za kuviepuka au kutafutia mbinu mbadala ya kuvishinda.

Comments

  1. Je unahitaji kujua chochote kuhusu Branding na Marketing? karibu

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

Baadhi ya vitu vinavyosababisha biashara nyingi kufungwa.

Umuhimu na maana ya Logo( Nembo) katika biashara yako.

Aina za malengo na mipango