Posts

Showing posts from July, 2014

Jinsi ya kuanzisha biashara bila ya kuwa na mtaji wa pesa. (Sehemu ya pili)

Baada ya kuangalia sehemu ya kwanza wiki iliyopita ya jinsi ya kujiajiri bila kuwa na mtaji pesa leo tunaendelea na sehemu ya pili. Kama imetokea umeshindwa kugundua kipaji chako bado kuna uwezekano wa kuanzisha biashara yako bila ya kuwa na mtaji pesa haya kitu cha kwanza ni unatakiwa ujitambue wewe ni nani kati ya mfanyabiashara au mjasiriamali halafu ona aina ya biashara ambayo ndani ya uasili wako mwenyewe  ichague kwa umakini halafu andika chini vitu ambavyo unavihitaji ili biashara yako ifanikiwe au ionekane andika pembeni ( Sio mpango biashara)halafu  anza kufanya utafiti wa hivyo vituulivoandika kwa kutafutia mbadala wake sehemu zote ambazo zinahitaji pesa ziorodheshe pembeni halafu anza kutafuta mbinu mbadala kwa kila kimoja usikurupuke chukua muda ili ufanye maamuzi mazuri kama ulichochagua kikondani ya sehemu  yako ya kujitambua kupata njia mbadala sio kazi ngumu.( Safari ya mafanikio huanzia mbali sana hakuna tajiri ambae alianza huku akiwa tajiri au alianza na mtaji mku

Nukuu za Chuma

Image

Jinsi ya kuanzisha biashara bila ya kuwa na mtaji wa pesa.

Imekuwa ni kawaida kwa watu wengi kutambua pesa kama mtaji wa kila kitu katika biashara , lakini katika ulimwengu wa biashara iko tofauti pesa sio mtaji bali pesa ni kiasidizi cha mtaji . Leo nitakupa baadhi ya njia unazoweza kutumia kuanzisha biashara yako bila ya kuwa na mtaji pesa ila kwa kutumia mtaji mbinu na vinginevyo. Watu wengi  huruka sana sehemu ya kwanza ya mtaji ambayo ndio  chimbuko la mtaji  na kukimbilia kwenye  sehemu zinazofuata na kuendelea bila kujua muhimili wa nyumba ni msingi bila ya msingi mzuri nyumba inaanguka hivyo bila chimbuko zuri la mtaji wako hauwezi kufanikiwa, sasa basi chimbuko hilo ni nini ambalo watu huliruka na kukimbilia mengine. Kichwa/ akili mtaji wako mkubwa ni kichwa chako na hata wazo na kila kitu kinaratibiwa na kichwa chako mwenyewe ndani ya kichwa ndipo panatengeneza ndoto na ndipo panapofanya ndoto zitimie kwa kushirikiana na viungo vingine vya mwili lakini injini ya mwanadamu ni kichwa katika kufanya mambo ya maamuzi. Kichwa ndi