Posts

Showing posts from December, 2019

Aina ya malengo ya kujiwekea unapomaliza mwaka

Image
 Wengi wetu inapofika mwisho wa mwaka hufikiria kuanza upya na kurekebisha sehemu tulizokosea ili mwaka unaofuata uwe wa mafanikio zaidi ya ule unaoishia ama kupita lakini malengo yetu huwa yanajichanganya sababu ya kukosa muongozo thabiti wa kuyafikisha mahala pake na mengi huishia kuwa matarajio ambapo matarajio yasipo kutana na malengo yanakuwa mawazo,wengi tunaangukia kwenye mawazo sababu hatupangi leo nakupa malengo ambayo unapomaliza mwaka hakikisha umeyaandika ili kukukuza wewe,biashara,kazi,imani na kadha wa kadha. hakikisha umezingatia maeneo makuu 7 tofauti ya kujiwekea malengo na kuhakikisha kila eneo unaweka mikakati thabiti itakayokuwezesha kufikia hayo malengo yako. Maeneo muhimu ya kujiwekea malengo ni: 1. Malengo ya Kiroho (Spiritual Goals) 2. Malengo ya Familia/Ndoa (Family/Marriage Goals) 3. Malengo ya Fedha (Financial Goals) 4. Malengo ya Maendeleo Binafsi (Personal Development Goals) 5. Malengo ya Kimwili/Kiafya (Physical/Health Goals) 6. Malengo ya Kazi (Ca

Hekima ya baba huonekana kwa mtoto

Image
HEKIMA YA BABA HUONEKANA KWA MTOTO Ukiwa mzazi mara nyingi hupenda kutumia ukali,fimbo na nyenzo kadha wa kadha katika kuwaelewesha watoto wetu Katika makuzi yao. Lakini leo nakupa changamoto kama mzazi kile kinachoonekana kwa mwanao ndio kile ulichokihitaji. Nadhana zinasema mtoto umleavyo ndivyo akuavyo lakini mimi ninaenda ndani zaidi ili kujenga zaidi,Hekima ya baba huonekana kwa mtoto,hivyo usipomfundisha hekima yako usitegemee yeye kujifunza kwa dunia. Wengi tumekulia malezi ya fimbo na ukali kiukweli zinasaidia lakini hazijengi Sana,fimbo zinatengeneza uoga,hofu,kutokujiamini,amri lakini hata uwezo mdogo wa kufikiri,haya na madhara ambayo huonekana baadae Sana hekima ya baba inakua ni uoga,hofu,kutojiamini na kadhalika ambapo vijana wa Leo ndio tatizo kubwa ufahamu ( mentality) zimeharibika tangu wakiwa wadogo,halafu wakifika ukubwani gafla wanatakiwa wajitegemee ni mtihani mkubwa zaidi kwao sababu hekima ya baba imepungua sana, tunakimbilia sana kuwalaumu watoto bila kutafuta c

Maisha huongeza thamani unapopita kwenye bonde la uvuli wa mauti.

Image
Mara nyingi mwanadamu akichomwa na mwiba ndio huona thamani ya kandambili (ndala) lakini kabla ya hapo zinaitwa malapa ya kuendea chooni. Hali hii imeendelea kwa vitu vingi tunavyovohisi muda mwingine ni vidogo na havina thamani lakini tunavihitaji sana,asilimia kubwa yetu uhai na pumzi tunayovuta tunaichukulia kawaida,kulala na kuamka salama tunaona kawaida kwa vile ni kitu kinachojirudia kila siku na wengine hata wanapopata matatizo hukimbilia hata kuwaza kwanini wanaishi ama maisha kwao hayana thamani,wanasindikiza wanaoishi na maneno kadha wa kadha,lakini siku unayopewa sababu ya kuona maisha yako yanakatishwa na kitu kifulani aidha ugonjwa,ajali,maradhi n.k ndio uthamani wake huja. Iko vivyo hivyo kwenye kila kitu unachokifanya kipe uthamani kabla hakijapotea elimu yako ni ya thamani sana usisubiri hadi ufe ndio tuone madaftari ya mipango yako mizuri,Anza kufanyia kazi ukiwa hai,Afya yako ni ya thamani usisubiri hadi uwe hospitali ndio uanze kuuona uthamani wake,Anza kuitunza afya

Elisha Chuma: Simamia wazo kuu

Wengi huwa tunakimbia wazo mama na kukimbilia mawazo mtambuka bila kukumbuka bila wazo mama mtambuka lisingeonekana. Simamia wazo kuu,unapelitenda wazo mtambuka hakikisha wazo kuu haliathiriwi. Elisha Chuma +255 745108010

Tofauti ya Ukweli na uhalisia

Ishi kiuhalisia endana na uhalisia wako,huenda ukweli unakuvuta ili usimame mahala ama kuonyesha uwezo lakini uhalisia ndio sehemu pekee unayoweza kuwa na amani na kutengeneza mafanikio yako. Watu wengi wamefeli kwa kuusimamia ukweli kuliko uhalisia mathalani,ukweli ni kwamba unahitaji kula ili uishi uhalisia ni kwamba unahitaji kufanya kazi ili upate hela ya kukuwezesha kununua chakula ili uishi. Wasanii,wafanyabiashara na watu wengi wamefelishwa sana na hiki kitu na bado kinawatafuna wengi kuung'ang'ania ukweli ilhali uhalisia unakataa ndio matokeo yake unaishi maisha yasiyokuwa ya kwako mwisho wa kuishi hivyo ni kufeli. Ishi maisha yako ya uhalisia utapata amani ya moyo na ni rahisi kutengeneza mafanikio na mbinu zake ukiwa kwenye uhalisia kuliko kwenye ukweli wako. #Maishanihayahaya #wakubadilikaniwewe