Posts

Showing posts from November, 2013

Hatua za kufuata unapofikiria kuanza ujasiriamali

Ujasiriamali sio kitu kidogo kama wengi wanavyofikiria na wengi hufikiria kupokea hasara ni kama vile umefungua duka hujauza vitu hadi muda wake wa kutumika umeisha   ndio unakuwa umepata hasara lakini kwa maana ya ujasiriamali maana iko tofauti kidogo maana ya kukubali hasara kwa upande wa ujasiriamali ni ile hali ya kukubali kutumia nguvu na gharama nyingi kwa ajili ya matokeo ya baadae ,ambapo matokeo hayo yanaweza kuchukua muda mrefu hadi yaonekane. Mjasiriamali ni mfanyabiashara pia na hakuna mfanyabiashara anaefanya biashara kwa hasara kila kinachofanyika katika biashara kinategemewa kulipa hata kama sio sasa, hivyo hata mjasiriamali pia hakubali hasara ila kwa malengo. Hivyo unapoamua kuwa mjasiriamali usikurupuke kwa vile unajiona unaweza kwanza kabla ya yote jitambue   kwanza (tofauti kati ya ujasiriamali na biashara),ukishakuwa na uhakika na hilo   sasa unaweza kuanza kufata hatua zifuatazo,nb: usifanye kwa kuwa unataka kujilazimisha kuwa mjasiriamali fanya kwa kufuata

Hatua za kufuata unapofikiria kuanza kufanya biashara yoyote

Watu tumezoea kudanganyana na kutokuelezana ukweli kuhusiana na biashara, tumekuwa watu wa kupeana moyo na kushauriana kila mtu afanye iashara lakini biashara au ujasiriamali sio kitu rahisi kiasi hicho ambacho kinaweza kufanywa na kila mtu. Hivyo usijitumbukize tu katika bishara kwa kufuata mkumbo aidha umeambiwa biashara fulani unaiweza, biashara fulani inalipa au wewe unaweza kufanya biashara fulani na ikakulipa, kila kitu kinaugumu wake na changamoto zake, changamoto za muuza maandazi ni tofauti na changamoto za muuza duka,hata ujuzi wa msusi ni tofauti na wa kinyozi japo wote wapo saluni,hivyo unapoamua kufanya biashara fulani usikurupuke fikiria na tathmini kwanza kwa undani kama inaendana na wewe zifuatazo ni baadhi ya njia au mbinu muongozo za kufuata unapotaka kuanza biashara yako. Wazo la biashara. Kitu cha kwanza unachotakiwa utafute ni wazo la biashara,hii itategemea na eneo pamoja na asili ya kazi yako (kwa muongozo wa jinsi ya kupata wazo la biashara.angal