Posts

Showing posts from November, 2017
Image
Kwanini unatakiwa kumuweka ndani mtoto mchanga siku 40 baada ya kuzaliwa. Muda na wakati unatupa mkono sana katika kuijua kweli na hii inasababishwa na vitu vingi mabadiliko ya uchumi,hali ya hewa,mitindo ya maisha,kuiga na vichocheo vingi vinatufanya tunabadilisha ile kweli kuwa kawaida, leo nitaongelea suala la kwanini mtoto anapozaliwa anatakiwa kuwekwa ndani kwa siku 40 ni kitu ambacho tumekikuta tumekirithi lakini tunakiacha, Je vizazi vyetu ama kizazi chako cha 4 kitafahamu kama kulikuwa na kuweka 40 kama kuanzia kwako haujaweka 40?. Historia,zama na ukweli vinatupeleka mbali sana lakini hii dhana ya 40 haijatumika kwa mtoto tu vipo vingi leo tutaangalia kwanini mtoto. Sasa basi katika mwili wa binadamu kuna kitu kinaitwa Aura hiki hauwezi kukishika wala kukigusa ni kama tabaka lililopo juu ya mwili wako ambalo linakusaidia na kukukinga na nguvu za nje,mfano unaweza kutembea ukahisi mwili umesisimka ghafla tambua hapo aura yako imefanya kazi,ama umepima na unaumwa lakini