Posts

Showing posts from 2015

MABADILIKO YA MFUMO: TAHADHARI KWA WAFANYABIASHARA NA WAJASIRIAMALI

Habari za leo wana Branding, nimelazimika kurudia kupandisha uzi huu kutokana na hali ya mabadiliko ya kimfumo na kiuchumi inavyoendelea hapa nchini, nimepokea maswali mengi kuhusiana na ishu ya mabadiliko yanayoendelea serikalini na kimfumo pia,majibu yangu hayakuwa mbali na tahadhari hii niliyoitoa mwezi Oktoba 2013 lakini leo imeleta majibu kwa kuanza kuonekana hebu pitia na uyasome tena kwa makini kwa maana bado mabadiliko yanaendelea kutokea.... tuwemo. Taa ya hatari imeanza    kuwaka kwa wafanyabiashara na wajasiriamali wa Tanzania Asilimia kubwa ya wafanyabiashara, ( wakubwa na wadogo) wanafanya biashara Kienyeji na kikubahatisha wanafanya biashara kama mchezo wa bahati nasibu kupata Kukosa    lakini siku sio nyingi mambo na hali itabadilika na kubadili mfumo wote wa kibiashara Hapa Tanzania. Kwa kuanza kwa sasa watanzaia wengi wanapata hamasa na hamu ya kuwa wafanyabiashara Au wajasiriamali kwa inspiration kutoka nchi za nje, kutoka kwa wajasiriamali wakubw

Aina za Brand

1.      Brand kama bidhaa Hufanya kazi ya ubora na thamani ya brand. Katika mkusanyiko wa matangazo ya bidhaa nyingi, mtumiaji huhitaji kujua jinsi ya kuchagua bidhaa moja juu ya nyingine, hivyo kwa kulinganisha udhania wake pale anapoamua kufanya hivyo huwa hana muda mwingi wa kulinganisha ,huamua kuchagua bidhaa ambayo inakidhi haja zake kutokana na brand. 2.      Brand kama mfumo/kampuni Hutengeneza muonekano chanya wa brand na huonyesha nyuma ya brand kuna mfumo Uwezo wa ushawishi wa kampuni hufanya bidhaa kuongeza thamani 3.      Brand kama mtu Hii hujishughulisha na uhusiano na wateja , hutengeneza kukutana kati ya mtu na brand Ni ngumu kuongeza soko kama hakuna mahusiano mazuri na wateja wako. 4.      Brand kama alama Hutoa muendelezo wa utambulisho wa brand Brand inayochukua akili yako hupata tabia , na brand inayochukua moyo wako hupata kujiapiza kwanzo.

Vitu vinavyoenda sambamba katika brand

Kuna vitu vitatu ambayo hutumika sambamba   ili kutengeneza brand yenye afya 1.      Logo - Nembo Nembo   ni alama maalum ya kwako peke yako inayokutambulisha sokoni na alama hiyo ndio Itakuwa inasimama kwa niaba ya kampuni yako 2.      Branding- kulijengea jina utambulisho Branding ni kutengeneza uaminifu na ahadi ya bidhaa yako kwenye akili ya mteja unaemtegemea Ambapo brand huunganishwa na bidhaa kwa mteja . 3.      Identity - utambulisho ( marketing,advertising,publication,sales) Hii inamaanisha aina ya utambulisho utakaotumia kujitambulisha, unaweza kujitambulisha kama expert Kujitambulisha kama mzoefu kujitambulisha kwa aina ambayo wewe itakupa ahueni na upenyo kwenye soko ulilopo. 4.      Kutokubadilika M oja ya vitu ambavyo vinatakiwa viangaliwe kwa umakini moja wapo ni kutokubadilika, brand inatengenezwa na utofauti wako katika eneo lako la ushindani hivyo kubadilika badilika ni kupotea uhalisia na uwezo wako wa ushindani kama biashar

Kazi za branding

Brand   hutambulisha muonekano ,ubora   wa kuaminika kwa watu, huku bidhaa za generic (kawaida)   hazijulikani   na haziaminiki ,hata hivyo brand ni ghali na inahitaji mipango ya muda mrefu Brand hutofautisha bidhaa na hufanya bidhaa kutambulika mapema Brand inaruhusu mtumiaji kutengeneza maamuzi na matumizi ya bidhaa Brand hutengeneza thamani halisi kwenye macho ya washirika wa kibiashara na hupenyeza thamani ndani ya macho ya mtumiaji Branding hutengeneza trademark ambayo huongeza thamani ya bidhaa.  Ungana nami zaidi kupitia ukurasa wangu wa facebook : Elisha  Chuma ("like" ukurasa huu na utapata habari zote na machapisho  mara tuu ninapotoa.) Asante

Maana ya Branding katika Biashara/ujasiriamali wako

Image
Brand ni rasilimali inayotokana na ahadi ambayo inaunganishwa na bidhaa kwa wateja wake. Au brand ni alama inayotambulisha nafasi yako kwenye soko lako la ushindani. Shughuli ya brand inatakiwa iwe imedizainiwa na kuandaliwa maalum   kwa ajili ya biashara yako k ukutofautisha na wapinzani wako kibiashara. Hata kama wapinzani wote wanamuonekano Mzuri au kukushinda wewe . 1.   Brand yenye mafanikio huzingatia sanaumoja, Inapojitambulisha haijitambulishi  kwa vitu vingi Mfano :1.   Kampuni ya Cocacola wanabidhaa nyingi lakini ukiona  matangazo yao wamejikita sana kwenye  kuitangaza cocacola  yenyewe. ikiwa inamaanisha japo wanabidhaa nyingi bidhaa  zote zinajitengenezea au zinatengenezewa brand yake yenyewe. 2.      Kuna tofauti kati ya mauzo na kubrand. Rolex Orijino Rolex feki Mfano: unaweza kuuza saa ya Rolex dola 100? Ni kweli inawezekana kuuzwa kwa bei hiyo    na zikauzwa nyingi lakini nini kitatokea baada ya muda mrefu kwenye bran