Posts

Showing posts from March, 2018
Image
Baadhi ya sehemu ambapo watu wengi wanafeli na kunyanyuka kwao kunakuwa kugumu  ni kati ya muumganiko wa kile anachokiwaza na uhalisia,na hii inachangiwa sana na kutengeneza mipango isiyokuwa na uhalisia wa maisha ama mzunguko wako wa maisha yako ya kila siku.Usitegemee kuja kufanikiwa kwa mpango ambao utaubadilisha zaidi ya asilimia 40 ya maisha yako ya kila siku,hakikisha mpango wako unazingatia uhalisia wa mzunguko wa maisha na uwezo wa kuufanya uwe hai.Simamia kuunganishwa kwake. Kitu kingine kinachowa rudisha nyuma watu wengi ni kuishi maisha ya wenzie,hata umempata roll model wako kamwe usitake kuishi kama anavyoishi yeye sasa hivi ukitaka uwe kama roll model wako anza kwanza kufatilia alifanya nini kabla ya kuwa kama alivyo usimuige kama alivyo sasa ila mfatishe alivyofanya hadi akawa kama alivyo sasa hivi.Kwenye akili unabeba ndoto kubwa ili uendane na roll model wako matokeo yake unafeli nakumfaidisha yeye. Pia kingine na kikubwa zaidi unatakiwa kujitambua ili mawazo