Posts

Showing posts from March, 2016

Jinsi ya kutafuta masoko kuendana na kasi ya ukuaji wa Teknolojia

Habari tena wanabranding, natumai mu wazima bukheri wa afya leo nimeona tukumbushane kidogo baadhi ya vitu ambavyo vitatusaidia wote kwa pamoja kuongeza masoko na kukuza uchumi wa taifa hili. Mada yetu leo inasema jinsi ya kutafuta masoko kuendana na kasi ya ukuaji wa teknolojia siku baada ya siku. Utandawazi umebadilisha mambo mengi sana katika maisha ya mwanadamu na miongoni mwa vitu ambavyo viliguswa ni pamoja na sekta ya biashara ambapo kadri mambo na siku zinavyoenda nayo inaenda inabadilika hasa kwa huku kwetu nchi zinazoendelea. Teknolojia imekuja kurahisisha baadhi ya kazi na utendaji kazi wa eneo fulani miaka ya nyuma ilikuwa kama unahitaji kusajili kampuni yako ni lazima uende Brela ukaandike jina, utume barua, wakujibu ndio uanze kuomba usajili lakini sasa hivi kila kitu unakifanyia nyumbani kwa kutumia kompyuta yako tu. Tra nao vivyo hivyo ilikuwa ni lazima uende ofisi zao ili kulipa kodi lakini sasa unaweza kutuma hata kwa simu, hayo ni baadhi ya mabadiliko ya teknoloj

Je! unajua maana ya Meme/Motto/Slogan katika biashara yako?

Watu wengi wamekuwa wanafanya vitu bila kutambua maana na kwanini, leo nitatoa dondoo kidogo kuhusu meme/Slogan/Motto. Hiki sio kitu kigeni lakini wengi tumwekuwa tukikifanyia mazoea leo pata darasa kidogo. Kila biashara inapofanyiwa branding lengo kuu liko kwa mteja na unapotaka kumpata mteja yoyote lazima uchanganye ahadi,ubora na picha. Ahadi hutolewa na Slogan au meme ya biashara, hivyo meme yako inamaana kubwa sana katika kuisimamisha biashara yako mfano. Katika magari Ukiwa unaendesha Marcedez Benz hata kama ni ya mwak 1921 bado slogan yake ni "expensive car" hata kama kiuhalisia sio kweli ila kwa vile brand yao ilitoa meme ya hivyo mteja anaweza kwenda kununua sio kwa sababu anaipenda Marcedez hapana ila tu ni kwa sababu its expensive car, gari aina ya BMW ni "comfortable car" nayo pia vivyo hivyo. Sasa basi nafikiri umepata picha ni kiasi gani meme inaweza kuathiri picha ya biashara yako aidha ukiifanya vibaya au vizuri. Chini hapa nakuwekea muongoz