Posts

Showing posts from October, 2017

Baadhi ya vitu vinavyosababisha biashara nyingi kufungwa.

Image
Leo nimepata nafasi ya kuandika waraka huu kwa ajili ya kuwakumbusha kidogo wafanyabiashara wenzangu na wajasiriamali wenzangu kuhusu dhana moja ya muhimu sana iliyopo katikati ya mauzo na kujitangaza. Biashara nyingi sana sijajua kama ni kwa sababu ya kutokujua misingi ya biashara ama kutokuwa na uelewa wa kutosha na biashara zinafanya mambo kinyume na vile ambavyo inatakiwa na kujikuta zinatumia gharama kubwa kutengeneza mauzo kuliko ambavyo ingapaswa kuwa. Mara zote huwa nikipita na nikiwa kwenye semina huwa nawakaumbusha wafanyabiashara wenzangu na wajasiriamali kwamba siku zote usiwekeze kwenye kutafuta mauzo tu, kumbuka na kulijenga jina ama picha ya biashara, kuna faida nyingi sana za kujenga jina /picha katika kichwa cha mteja wako,lakini biashara nyingi hazifikirii sana kuhusu hilo bali wanawaza kuongeza mauzo tu. Siku zote mauzo ni mazuri lakini mauzo bila ya kuwa na jina ni gharama,nimeshakutana na wateja wengi sana wenye kutumia kauli hii " Mimi ninabi