Posts

Showing posts from April, 2020

Jiandae kufeli

Image
Biashara,Mahusiano,Mipango mingi inafeli sababu watu hawajiandai na changamoto za anachokitafuta ama kukifanya matokeo yake anawaza faida tu,zinapokuja changamoto zake anajikuta anafeli kirahisi sana Biashara nyingi zinapoandaliwa huwa ni kw mpango wa "high season" mauzo yako juu lakini uhalisia hakuna biashara ambayo inakuwa kwenye high season mwaka mzima ni lazima kuwe na kipindi cha "low season" mauzo hafifu na hapo ndio biashara nyingi hufa,kwa kuwa hazikujiandaa na low season matokeo yake ni kula mtaji na kupumzika,hili ni janga la biashara nyingi...UNAPOTENGENEZA MPANGO WAKO WAZA NA KIPINDI CHA KUFELI AMA KUPOROMOKA KWA BIASHARA UTAFANYA NINI?. Kwenye mahusiano wapenzi wengi huingia wakitegemea raha tu na furaha na mara nyingi mwanzo wa mahusiano kila mtu hujitahidi kufanya ili kumridhisha mwenzake,ila baada ya muda ile hali ya kuridhishana huisha huingia hali ya uhalisia hapo ndio shida huanza,vikwazo,wivu,husda,vijitabia huonekana,sasa kwa kuwa akili ya weng

Mafanikio na gharama zake.

Image
Nimekuwa nikikutana na kujadiliana na watu wengi sana kuhusu mbinu na jinsi ya kufanikiwa,nimegundua watu wengi wanayapenda sana mafanikio na wanatamani kufanikiwa lakini hawakotayari kuzibeba gharama za mafanikio hayo. Kufinikiwa ni kupiga hatua na hakuna hatua inayopigwa bila kutumia nguvu,hata hatua ya mguu wako ili unyanyuke unahitaji nguvu,balance,uelekeo na mambo kadha iko hivyo pia kwenye mafanikio. Ili ufanikiwe lazima uzikubali gharama za eneo lako la mafanikio,usiwe kwenye kundi la kutamani kila siku na ku"wish" jitoe kwenye hiyo hali kwa kubadilisha mawazo yako. Na ili ufanikiwe utakavyo tumia gharama kutengeneza mafanikio yako,usiombe kila kitu wakati wewe unatengenezewa kitu. Mafanikio yanaanza na mabadiliko ya tabia na mtazamo,anza kufanikiwa ndani yako sasa ili uyatengeneze mafanikio ya nje. Elisha Chuma. Mwalimu,Mshauri & Kocha wa Mafanikio