Posts

Showing posts from October, 2016

IPENDE BIASHARA YAKO

Image
Hakuna kitu kizuri kama kuitangaza biashara yako kitaalamu na kwa mvuto zaidi, biashara zote zinalipa ila inategemeana na unaipenda biashara yako kiasi gani, tujenge mazoea ya kurudisha kwa ajili ya biashara mfano, unapotangaza viatu,mafuta ama nguo hata kama sio vya kwako ila ukitengeneza na nembo yako ukawa kila unachopost kinakuwa nayo hautengenezi muonekano tu bali unatengeneza na hadhi pia, asilimia kubwa ya biashara tuzifanye kwa ajili ya vizazi vijavyo pia bila kuwa na msingi hata wa muonekano biashara inamaanisha ukichoka na yenyewe inachoka lakini kukiwa na msingi hata wa page rasmi ya bidhaa ni rahisi kuendelezwa,pia inapoteza uzito unapotangaza unauza kitu mathalani cha laki 1,2 hadi milioni ila umekipiga picha tu na simu yako hata hakionekani vizuri,tengeneza muonekano wa biashara yako leo ili ujisaidie mwenyewe na vizazi vijavyo. Tengeneza nembo yako vizuri iwe na muonekano thabiti ili ikidhi vigezo za kada yako,dizaini mtindo ambao utautumia kujitangaza ama

Biashara hatua 6 za kukuongoza kutengeneza brand yako kwa kiwango ulichopo ( Sehemu ya 3)

3. Chagua sehemu sahihi ya kujibrand Kila biashara inasehemu yake ambayo inajitosheleza hata biashara yako pia inasehemu ambayo ukiiweka inatosha kabisa hivyo chagua kwa makini sehemu ambayo unaiweka biashara yako ili usije kupishana na biashara yako. Ili kujua sehemu sahihi ya kuiweka biashara yako no lazima utambue vitu vifuatavyo ili kukupa mwanga wa unakoelekea. 1. Aina ya wateja wako 2. Hali zao kiuchumi 3. Wanapatikana wapi 4. Unawapataje 5. Nnatumia mbinu gani? Ukishayajibu maswali hayo kwa ufasaha utatambua eneo lako ambalo ni sahihi kujitangaza japo kwa hali ya sasa teknolojia ndio sehemu ambayo wateja wengi wanapatikana hata huko pia kuna matabaka, wateja walioko Facebook ni tofauti na wateja walioko Linkeldin na tofauti na wateja walioko Instagram hivyo usikurupuke kwa kufuata biashara ya mwenzako kwamba kwa vile alifanya kupitia kile akafanikiwa na mimi basi nitafanikiwa hapana utafeli sababu kila biashara ina njia zake za kutokea. leo nitaishia hapa toleo lij

Biashara hatua 6 za kukuongoza kutengeneza brand yako kwa kiwango ulichopo ( Sehemu ya 2)

2. Anza kujirasmisha  Kabla ya kuingia sokoni ni vizuri sana ukiwa umejirasmisha nikiwa namaanisha ukiwa umejiweka rasmi kwa kuingia katika ushindani maana biashara ni ushindani usiposhinda basi utakuwa hauna nafasi katika biashara hiyo ambapo kwako ambae ndio mgeni ama mchanga katika hilo usipojirasmisha mapema inamaanisha unaenda kufeli pale utakapokutana na washindani wako ambao tayari wapo kwa muda mrefu na wamejirasmisha ukiingia kichwa kichwa utajikuta unatumia gharama kubwa kupata nafasi katika soko ambapo ilikuwa ni rahisi kwa kujirasmisha na kutumia upenyo wa soko ambao umeiweka biashara yako. Nnaposema kujirasmisha nnamaanisha ni kutengeneza vitu ambavyo vitakuweka rasmi katika soko, vitakupa uhalali wa kuwa sokoni na baadhi ni vitu ambavyo mteja atahitaji avione mwanzoni pale anapokutana na biashara yako ambavyo kwa ushauri wangu  ni pamoja na 1. Logo ( Nembo) 2. Businesscard 3. Identification( Vitambulisho) 4.  Letterhead( kichwa cha barua) 5.Envelope

hatua 6 za kukuongoza kutengeneza brand yako kwa kiwango ulichopo ( Sehemu ya 1)

Watu wengi wamekuwa wakiniuliza swali la napotaka kuanza kufanya Branding natakiwa nifanye kitu gani?, kitu cha kwanza ambacho ni msaada mkubwa kwako kwanza unatakiwa uijue Branding yenyewe ni nini, ndipo unaweza kutambua unatakiwa kuanzia wapi kisha ukaelekea wapi, lakini kwa kupunguza muda na kusaidia kuokoa wakati unaweza kufanya hivi. 1. Tengeneza brand plan Kitu cha kwanza ambacho unaweza kufanya unatakiwa uwe na mpango wa kila kitu unachokifanya usifanye kwa kukurupuka kwa vile watu wengine huwa wanafanya hapana utakuwa unakosea unatakiwa utengeneze mpango wa jinsi ya kujibrand,ili ukuongoze kwa hatua kulingana na soko lako pia malengo na maono ya biashara yako. ukiwa na brand plan itakusaidia kupata mwanga wa nini cha kufanya,wapi na kwanini. Brand plan inakusaidia wewe mwenyewe kuona mwanga wa biashara yako inaenda wapi inaongozwa na nini na ina sehemu gani katika soko, hivyo unapoitengeneza tayari unapata mwanga wa kutosha wa biashara yako pia inakusaidia kutengeneza baj