Posts

Showing posts from March, 2014

Kuongeza uelewa

Habari za Jumatatu baada ya kutoa maelezo ya njia na baadhi ya hatua  za kufanya katika biashara wiki hii nitakuwa ninapokea maswali kuhusiana na mada zangu nilizoandika hapo awali kama kuna sehemu umepata utata unaruhusiwa kuuliza kwa kutumia comment chini ya huu uzi au kwa kutuma email moja kwa moja kwangu kupitia elishachuma@gmail.com. Huduma hii itakuwa ni ya wiki 1 ( siku 7)

Tofauti kati ya Branding na Marketing ( Masoko)

Kumekuwa na Mkanganyiko wa matumizi pia ya hivi vitu viwili Branding na Marketing ( Masoko) na imekuwa ni tatizo kugundulika ipi inayotakiwa ianze kati na ipi ni kubwa zaidi ya mwenzake . kwa upande wa Branding tayari nilikwisha elezea kwenye toleo za nyuma  Branding . Leo nitaelezea kidogo maana ya masoko na tofauti yake na Branding Masoko (Marketing)   ni kila mkutaniko wa kampuni yako na mtu au kitu chochote duniani Maana ya marketing ( Masoko) inajumuisha; Jina la biashara,mgawanyo wa aidha unatoa huduma au bidhaa,njia za utengenezaji au utoaji huduma,rangi,saizi na umbo la bidhaa yako,upakiaji,eneo la biashara,kujitangaza,mahusiano na jamii, tovuti,Branding,email,sahihi yako kwenye majarida na chochote unachokitoa ,ujumbe wa sauti,matamasha ya mauzo,simu,mafunzo ya uuzaji,jinsi ya kutatua matatizo, mipango endelevu ,watu wanaokuwakilisha,wewe,unavyofuatilia Lakini pia kwa upande mwingine marketing(Masoko) inajumuisha,wazo kuu la brand yako,huduma yako,mueleke

Ukweli kuhusu ujasiriamali

Nimeshaandika sana kuhusiana na ujasiriamali japo sijafikia sehemu ambayo inatakiwa lakini inatakiwa tufikie hatua tuache kudanganyana kuwa mjasiriamali sio suala dogo   lakini watu wamefanya kama vile ni kitu ambacho kila mtu anaweza kukifanya, ujasiriamali sasa umekuwa ni wimbo kila mtu ni mjasiriamali hata muuza vitumbua nae ni mjasiriamali tunapoteza vijana wengi kwa wadanganya kuhusiana na ujasiriamali , ukweli ujasiriamali ni mgumu na tena sio mgumu kidogo ni mgumu sana. Ukianza kiuangalia nadharia ya ujasiriamali   ni mtu mwenye ujasiri na nguvu kwenye mali lakini tofauti na ambavyo tunauangalia kwa upande mwingine ambavyo ndivyo asilimia kubwa wanafahamu kwamba ujasiriamali ni uwezo wa kufanya au kumiliki biashara yako , huo ni uongo tena mkubwa, tunakopi vitu kutoka nchi zilizoendelea halafu tunatafsiri vibaya , ukiangalia watu wanaoitwa wajasiriamali kwa nchi za nje ni tofauti kabisa na wanaoitwa wajasiriamali wa huku, na kitu kibaya zaidi ni kwamba tunakopi mifano ya

Semina ya Mafanikio

Hatimaye siku imefikia,leo ndio mwanzo wa semina yetu inayoanza leo na kuendelea hadi mwaka mzima (miezi 12) baadhi ya mada zitakazofundishwa kwa undani ni pamoja na                                     Kujitambua Jinsi ya kupata wazo la biashara Mawazo 100 ya biashara Mpango mkakati wa biashara yako Vitu unavyotakiwa kuvifanya unapokuwa mjasiriamali au mfanyabiashara. Nguzo kuu 5 za biashara na mafanikio yako Na mengine mengi. Karibu sana kwa ajili ya semina hii ya mafanikio kwako na biashara yako, bado unaweza kujiunga na kuendelea na semina hii,semina sio ya mkoa au sehemu moja au nchi hii ni kwa wote wanaotumia mtandao kote nchini na hata nje ya nchi ukijiunga na semina hii utapokea makala za Elisha Chuma na mafunzo maalum kwa njia ya email na ukiwa na ukiwa na tatizo au swali unaweza kunitafuta kwa simu au email na nitakujibu haraka iwezekanavyo. Leo tunaanza na mafunzo ya kujitambua mwenyewe kama unachokifanya kinaendana na wewe au unafanya bila kujitambua ilimradi u

Vitu 10 (Kumi) vitakavyofanya biashara yako ifanikiwe

Image
Bishara yako haiwezi kujiendesha yenyewe bial kuwa na vitu vinavyoisimamia leo nimekuletea vitu 10 vitakavyoifanya biashara yako ifanikiwe, ni vitu ambavyo tunaviona ni vidogo na vipo katika maisha yetu ya kila siku hivyo tunavifanyia mazoea lakini sasa 1. Ipende biashara yako. Biashara yako ni maisha yako ndio mfereji wa kipato chako hivyo inatakiwa ipendwe na kuthaminiwa,unapoweka upendo wa kutosha kwenye biashara yako lazima mafanikio yatakuja yatakayokuja, fanya biashara kwa upendo na moyo wa kujituma.usifanye biashara yako kama ya jirani yako ipende na ithamini itakupenda na itakulipa. 2. Jenga uamninifu. Katika biashara kitu cha muhimu kuliko yote ni uaminifu sababu mteja anapokuja kununua au kupokea huduma kutoka kwako ni kutokana na uaminifu kwako na kuamini huduma yako hivyo   fanya kazi kwa uaminifu sikuzote kwa mafanikio na maendeleo ya biashara yako.Uaminifu wako ndio mafanikio yako fanya kila kitu kwa uamnifu . 3.  Usibadilike bad

Muendelezo wa hatua za kutengeneza mpango biashara ( Business plan)

Image
Mara ya mwisho tuliangalia hatua sita (6)za mwanzo katika shughuli hii ya kutengeneza mpango biashara (business plan), leo tutamalizia hatua sita nyingine zilizo baki.hatua za mwanzo zilikuwa no pamoja na Jina,Aina ya biashara,Historia ya biashara na maendeleo yake,Huduma/bidhaa,Tathmini ya soko na Ushindani. Leo tutazimalizia zilizobaki kwa kufuata utaratibu. Masoko Katika mpango biashara wako unatakiwa uonyeshe mbinu za  promosheni na mauzo ya bidhaa/ huduma yako na vitu unavyotakiwa uvitolee maelekezo zaidi ni pamoja na muonekano wa ya huduma/bidhaa yako, utofauti wake, utambuzi wa wateja wako,watu wanaofanya kazi za masoko  na mauzo,mzunguko wa mauzo, aina ya kujitangaza/promosheni, Upangaji wa bei, Ushindani na huduma kwa wateja. Ufanyaji kazi Kipengele  hiki unatakiwa uonyeshe uelewa wako wa kufuatilia maendeleo ya huduma/ bidhaa kutoka katika uzalishaji hadi kwenye soko na baadhi ya vitu vya kuainisha ni pamoja na Gharama za mtindo wa uzalish

Utaratibu na Majibu (Semina)

Nimepokea maswali mengi na maoni mengi kuhusiana na utaratibu wa kulipia na kuipata semina hii na kutokana na sababu hizo muda wa kuanza semina umesogezwa mbele Semina itaanza rasmi : 15/3/2014 lakini haitakuwa na shida hata kwa uliyechelewa ukijiunga utatumiwa mada zilizopita na maelezo ya wenzako walipofikia. Utaratibu wa malipo ni unatuma pesa kupitia simu ya mkononi kwenda namba 0684 047323 au 0767603699 na ile namba ya muamala utakayopewa utaituma tena kwenda namba hiyo hiyo pamoja na email yako kisha utapokea meseji yenye utambulisho wako  kwa ujumbe wa meseji pamoja na email hapo tayari utakuwa umeunganishwa na huduma hii. Tafadhali jiunge mapema ili tuanze pamoja semina hii ya masomo muhimu kwa ajili yako na biashara yako.kwani unapochelewa utapokea tu mrejesho wa somo ila hautapata wasaa mzuri wa kulielewa somo. Kwa maswali na maelekezo zaidi tafadhali wasiliana nami kwa namba tajwa hapo juu. Asanteni na karibuni sana