Elimu inayokosekana


Elimu inayokosekana na inayowapoteza wengi katika maisha

Katika mfumo wetu wa elimu kuna elimu muhimu inayokosekana  na hakuna sehemu ya kuipata hadi
Ujitambue mwenyewe ambapo  elimu hiyo ni elimu ya kujitambua,

Tatizo lililopo katika elimu yetu ni kwamba tunasoma kwa kufuata taratibu za watu fulani, mfumo wa elimu tunaotumia
Ni wa mzungu , ili ujikomboe unatakiwa ujitambue, mzungu alileta elimu lakini haikuwa elimu ya kutufanya tujitegemee
Elimu tunayoipata kwenye shule zetu kuanzia ngazi ya chekechea hadi ngazi ya sekondari ni elimu ya lugha na kusoma na kuandika, kama ni hivyo kwa nini basi tuendelee kupoteza muda wingi kusumbukia kusoma na kuandika?.

Wanafunzi wanachukua hadi masomo 14 yote ayafanyie mtihani na anatakiwa kufaulu ni uwezo wa hali ya juu unaotumika kwa wanafunzi wanaofaulu, na hicho hakikuwa kizazi cha dot.com ambacho kila kitu wanafunzi wanatumia
Mbadala wa google kutafuta.hata kufeli sana kwa wanafunzi wetu kumesababishwa na mabadiliko ya hali ya utandawazi
Nchini zamani ilikuwa ili ufaulu unajitahidi kujisomea sana na kujisomea kwenyewe ni  kwa makatasi ya mitihani iliyopita na vitabu lakini sasa hivi hali ni tofauti hadi wanafunzi  wa shule za msingi wameshakuwa watumwa wa kompyuta kila kitu wanajua kinawezekana hata wanaoshindwa wanajua google itawasaidia lakini. Waliofanya na kusoma kabla ya google walifaulu vipi?

Serikali imekazania sana masomo ya sayansi na hakuna sayansi wanayoisoma tofauti na historia ya sayansi, maabara zenyewe sio za kutosha lakini katika mtihani unatakiwa ufanye nadhalia na vitendo ni jambo gumu kwa wanafunzi wetu na katika hilo bado serikali inataka mtu ajitegemee atajitegemea kwa kitu gani iwapo mmeshamfanya awe tegemezi.

Mfano: Mwanafunzi akiwa msingi kapata elimu ya kusoma na kuandika hadi akamliza huku somo moja tu ndio anafundishiwa lugha ya kigeni, kaingia sekondari lugha inabadilika sasa ni somo moja tu ambalo anafundishiwa lugha ya nyumbani ( hapo tayari umeshamchanganya ni sawa na umemrudisha kuanza msingi wakati yuko sekondari) tena anachukua masomo 14 masomo yote hayo anatakiwa ayaweke kichwani mwake aidha yanamsaidia au hayamsaidii katika maisha ( wakati maana ya kusoma ni kupata elimu amabayo itakuja kukusaidia mbeleni katika maisha yako, kuna umuhimu gani kusoma masomo yasiyo kusaidia ).bila kumuandaa au kumpa machaguzi kulingana na atakachosoma ( mfano: CBG,PCB - Haya kwa upande wa sekta ya afya ,hkl,hgl - haya kwa upande wa lugha ) mwanafunzi anaanza kujichagulia bila kuwa na uchaguzi hivyo uchaguzi wake utafuata ashauri wa marafiki au kundi fulani , aatachukua
Hayo masomo na ataendelea nayo hadi chuo , lakini kutokana na kuwa hayakuwa katika mipangilio yake ya maisha ya baadae ndio unakuta mtu anadegree ya sheria ila anaomba kazi ya kuwa administrator.

Serikali haiwaandai wanafunzi kutambua tofauti iliyopo pale ambapo mtu akiwa shule, akiwa chuo, akiajiriwa na anapo jiajiri mwenyewe, hakuna elimu hiyo lakini baada ya kuona vijana wengi wanapotea sasa hivi vijana wanashauriwa wajiajiri watajiajiri vipi wakati hawana hata hiyo elimu ya ujasiriamali?.

Inatakiwa watu wajitambue ilhali wakiwa bado wanauwezo wa kukunjika sio tayari wameshanyongorota ndio mnaanza kuwaambia wajinyooshe, elimu ya kujitambua inatakiwe itambulike kwa kila mtu kuanzia mtoto hadi mtu  mzima ikiwa unajitambua hauwezi kukaa mtaani miaka nenda rudi bila kupata kitu cha kufanya kutokana na elimu uliyoipata lakini kwa sababu hajafundishwa kujitambua, muda wa yeye kujitambua anakuwa tayari anamajukumu mengine tayari hiloni tatizo .

Ushauri wangu.
Yafaa serikali kuanzisha masomo au kuwe na vipindi maalum katika mtaala wa elimu kufundisha elimu ya biashara na ujasiriamali kwa wanafunzi wetu ili wanapohitimu tayari wanakuwa wameshajitambua wako upande gani. Pia ushauri wangu serikali ipunguze masomo yasiyokuwa na umuhimu kwa mwanafunzi anapoteza muda mwingi kufanya yasiyo na manufaa katika maisha yake.

Comments

Popular posts from this blog

Baadhi ya vitu vinavyosababisha biashara nyingi kufungwa.

Umuhimu na maana ya Logo( Nembo) katika biashara yako.

Aina za malengo na mipango