Hali za kimaisha za vijana zisitumike kama mtaji wa kisiasa kwa vyama na wanasiasa.



Nukuu za Elisha Chuma

Kwanza kabisa nitoe shukrani zangu za dhati kwa wewe ambae umeendelea kunitumia ujumbe mfupi ,kunipigia simu na kunitumia barua pepe kwa ajili ya shughuli hii,siwezi kuwataja wote kwa majina lakini ninautambua mchango wenu bila kusahau wapenzi wa blogu hii ambao huendelea kutembelea blogu hii hata kama sijaweka uzi upya niwashukuru kwa namna ya kipekee kabisa.

Baada ya kupita kimya kidogo cha kutokuwa na uzi nimeonelea kwanza leo tuzungumze kidogo na vijana wa taifa hili maana hakuna familia isiyokuwa na kijana au vijana katika nchi hii, hata kama hatakuwepo kijana basi kutakuwa na kijana mtarajiwa.Tuko katika kipindi cha uchaguzi hivi sasa na watu wengi wanajitahidi kupata nafasi au sehemu ya kujishikiza kwa kipindi hichi ili angalau na wao wapate japo kidogo kitu katika mzunguko huu wa kampeni na mchakato wa uchaguzi kama mlivyoona kwa sasa kuna kampeni na zoezi la uandikishaji wapiga kura ambapo zinatumika mashine za BVR asilimia kubwa ya waandikishaji ni vijana hivyo katika kipindi hiki vijana watapata sana ajira za muda mfupi kwa ajili ya uchaguzi.

Lakini dhumuni langu kutoa uzi huu ni kuwakumbusha tu vijana wasitumike kama mtaji wa kisiasa aidha kwa chama au kwa mwanasiasa, tuko katika kipindi cha uchaguzi mkuu wa serikali asilimia kubwa ya watendaji wakuu wa serikali wanaenda kubadilika kupitia uchaguzi huu hivyo asilimia kubwa ya mipango mipya na ahadi za zamani zinakuwa zimefikia kikomo kwa sasa labda tu kukamilisha utaratibu wa zile zilizoanza kabla,lakini kumekuwa na wimbi kubwa la misaada na mipango chanya kwa ajili ya vijana na wajasiriamali wadogo kwa ajili ya kuwasaidia kuwainua kiuchumi.

Nnawaasa vijana kuwa makini na fursa hizi kwani nyingine ni kwa ajili tu ya uchaguzi na kampeni hivyo wanaweza kupoteza malengo yao ya muda mrefu ambayo wamejiwekea kwa kujiingiza katika kitu cha muda mfupi ambacho kitakugharimu muda mrefu baadae,

Ushauri kwa serikali.

Serikali inajua takwimu za vijana wanaobaki na wanaoingia kazini kwa mwaka
Takwimu zinaonyesha kila mwaka wanahitimu vijana kati ya 800,000 –1,000,000 lakini nafasi za kazi zinazotakiwa ni kati ya 400,000 hadi 600,000 hivyo hadi hapo tayari inaonyesha kila mwaka tunaidadi kubwa ya vijana ambao wamesoma lakini hawana ajira kila mwaka.Serikali itafute au itengeneze mfumo thabiti ambao utasaidia nchi kuwa na usawa na uhalali katika suala la elimu na sio kushusha viwango vya ufaulu ili tupate wahitimu butu kwa ajili ya kazi zenye makali,

Nafikiri serikali iongeze makali katika viwango vya ufaulu na wanafaulu pia wafaulu kihalali na wanaofeli pia wafeli kihalali lakini itambulike tu hakuna mtu asiekuwa na msaada kwa mwenzake leo hii dunia nzima waliosoma wanafanya kazi kwa wasiosoma hivyo,serikali inaweza kutengeneza hata vyuo vidogo vidogo kwa ajili ya kuwapokea wanafunzi waliofeli na kuwapa masomo na maandalizi ya jinsi ya kuishi na ujuzi wa vitu nje ya shule na nyumbani ambapo kama kijana akipewa elimu sahihi akitoka hatakwenda kujibweteka tena na kusubiri second selection au kwenda kusubiri aliesoma amalize ili amsaidie sababu atakuwa na chachu na mafunzo thabiti ya nini cha kufanya sehemu aliopo, ambapo na alisoma akimaliza atakuta sokoni kazi za weledi wake zinamsubiri hivyo  ataingia moja kwa moja kazini tofauti na sasa mwenye weledi wa dokta anafanya kazi ya udreva.

Comments

Popular posts from this blog

Baadhi ya vitu vinavyosababisha biashara nyingi kufungwa.

Umuhimu na maana ya Logo( Nembo) katika biashara yako.

Aina za malengo na mipango