Hatua za kufuata unapofikiria kuanza kufanya biashara yoyote
Watu tumezoea
kudanganyana na kutokuelezana ukweli kuhusiana na biashara, tumekuwa watu wa
kupeana moyo na kushauriana kila mtu afanye iashara lakini biashara au
ujasiriamali sio kitu rahisi kiasi hicho ambacho kinaweza kufanywa na kila mtu.
Hivyo usijitumbukize tu katika bishara kwa kufuata mkumbo aidha umeambiwa
biashara fulani unaiweza, biashara fulani inalipa au wewe unaweza kufanya
biashara fulani na ikakulipa, kila kitu kinaugumu wake na changamoto zake,
changamoto za muuza maandazi ni tofauti na changamoto za muuza duka,hata ujuzi
wa msusi ni tofauti na wa kinyozi japo wote wapo saluni,hivyo unapoamua kufanya
biashara fulani usikurupuke fikiria na tathmini kwanza kwa undani kama
inaendana na wewe zifuatazo ni baadhi ya njia au mbinu muongozo za kufuata
unapotaka kuanza biashara yako.
- Wazo la biashara.
Kitu
cha kwanza unachotakiwa utafute ni wazo la biashara,hii itategemea na eneo
pamoja na asili ya kazi yako (kwa muongozo wa jinsi ya kupata wazo la
biashara.angalia matoleo ya nyuma),hakikisha wazo ulilolipata linaweza
kukupa mafanikio, usitumie wazo la kujaribu kuna watu hufanya biashara kwa
kujaribu yaani anafanya kuijaribu biashara kama itamlipa, ukifanya biashara kwa
mtindo huo haiwezi ikakulipa na haiwezi kukua mafanikio yake yatakuwa hafifu
sana.
- Utafiti wa kwanza
Baada
ya kuchagua wazo bora la biashara usikurupuke kuanza kwa sababu umepata wazo
zuri na bora la biashara basi ndio unaanza mara moja,hapana mara nyingi
unapotengeneza wazo huwa unatengenezea na faida hivyo ukiwa na wazo faida ni
nyingi kuliko matumizi hivyo usikurupuke kitu kinachofuatia na kuanza kutafiti, fanya utafiti kama kuna
mtu au sehemu nyingine kuna biashara
kama unayoitaka kuifanya nenda fanya utafiti kwa kupitia biashara yake, ongea
nae akueleze ni changamoto gani anapata,kiwango cha faida,hasara,gharama,ugumu
na pia mbinu zake,kama hakuna mtu anaefanya biashara kama hiyo anza kufanya
utafiti kupitia mtu wa mwisho kupokea bidhaa yako, utafiti wa
- Bajeti = Fanya utafiti wa bajeti yako unatakiwa iweje ili ukamilishe na kuifanya biashara yako ianze na afya.
- Muda = Fanya utafiti wa muda, ni muda gani utatumika kuanzia katika utafiti wako wa kazi hadi kufika katika mafanikio yako.
- Nguvu kazi = Fanya utafiti wa aina na uwezo wa nguvu kazi inayohitajika katika biashara yako ili pia utengeneze na mfumo mzuri wa hiyo biashara.
- Vifaa = Fanya utafiti wa vifaa vitakavyotumika gharama zake, uwezo wake na uimara ili ujue ni kifaa kipi kitakufaa na kipi hakitakufaa.
- Faida = Fanya utafiti wa faida yake,kulingana na uhitaji wa wateja watarajiwa hii itakupa muelekeo wa biashara yako kama italipa mapema au itachukua muda, kama itakugharimu sana au itaanza kujihudumia mapema.
- Washindani = Fanya utafiti wa washindani wako pia wa aina zote tatu na uione nafasi yako kwao je? ukianza biashara utakuwa tone la maji baharini au mafuta kwenye maji,angalia mbinu zao uwezo wao na mapingufu yao.
- Eneo = Eneo litakalofaa kwa aina ya biashara yako na mbinu zako
- Mpango biashara
Baada
ya kufanya utafiti huo utakupa mwanga wa ni kitu gani kinahitajika na nguvu kiasi gani
itakuweka usimame unapopahitaji,sasa kinachofuata ni kutengeneza mpango
biashara ( Business plan) ambayo ndiyo itakuwa kama muongozo wako kwa kipindi
husika,baadhi ya vitu utakavyoainisha na kuvifafanua katika mpango biashara
wako ni pamoja na .
- Utafanyaje = Hii ikiwa inamaanisha utendeji wako wa kazi utakuwaje na utaupeleka namna gani
- Muda =Utaonyesha muda wa kuifanya hiyo kazi na jinsi itakavyofanyika
- Mbinu = Kwa vile umeshatambua washindani wako na umeshatambua udhaifu wao tengeneza mbinu ambazo zitakuwa haziwaakisi moja kwa washindani wako ila zinawaathiri baada ya muda.
- Washindani = Orodhesha washindani wako na uandike mbinu utakazotumia kupambana nao,
- Mipango = Tengeneza mipango ya biashara yako ambayo utaifanyia kazi ili kufikia mpango mkubwa, mipango hiyo iangalie uwezo na kasi ya biashara ili isije kuwa juu au chini ya kiwango cha biashara yako kuna mipango ya muda mrefu na muda mfupi,Fanyia mipango yote.
- Utafiti wa 2
Baada
ya kutengeneza mpango biashara yako sasa fanya utafiti mdogo wa mpango biashara
yako kama ukiiweka sokoni italeta mafanikio au haitaleta mafanikio,kwenye
ulimwengu wa biashara kuna tofauti kubwa kati ya mawazo na kitu/hali halisia.
- Ukiona unanafasi katika biashara hiyo basi fanya na anza mara moja kwa kufuata muongozo wako ulioutengeneza hapo awali,kama unaona nguvu yako ni ndogo kulingana na soko na ulivyojipanga,badilisha mpango uendane na soko pamoja na uwezo wako.
Nukuu:1. Uwezo na nguvu ni akili,fedha ni
mwezeshaji tu.
2. Kuna tofauti kubwa kati ya wazo
na kitu halisi jitahidi kusimamia na kufanya ulichokiwaza
mwanzo
3. Ujasiriamali na biashara sio kitu
cha kujaribu.AMUA fanya,jaribu ACHA
Comments
Post a Comment