Hatua za kufuata unapofikiria kuanza ujasiriamali


Ujasiriamali sio kitu kidogo kama wengi wanavyofikiria na wengi hufikiria kupokea hasara ni kama vile umefungua duka hujauza vitu hadi muda wake wa kutumika umeisha  ndio unakuwa umepata hasara lakini kwa maana ya ujasiriamali maana iko tofauti kidogo maana ya kukubali hasara kwa upande wa ujasiriamali ni ile hali ya kukubali kutumia nguvu na gharama nyingi kwa ajili ya matokeo ya baadae ,ambapo matokeo hayo yanaweza kuchukua muda mrefu hadi yaonekane. Mjasiriamali ni mfanyabiashara pia na hakuna mfanyabiashara anaefanya biashara kwa hasara kila kinachofanyika katika biashara kinategemewa kulipa hata kama sio sasa, hivyo hata mjasiriamali pia hakubali hasara ila kwa malengo.

Hivyo unapoamua kuwa mjasiriamali usikurupuke kwa vile unajiona unaweza kwanza kabla ya yote jitambue  kwanza (tofauti kati ya ujasiriamali na biashara),ukishakuwa na uhakika na hilo  sasa unaweza kuanza kufata hatua zifuatazo,nb: usifanye kwa kuwa unataka kujilazimisha kuwa mjasiriamali fanya kwa kufuata origin yako.



  1. Kutambua investment unayoiweka
Unapokuwa mjasiriamali ni  sawa unakuwa unatengeneza mpango wa kifo chako au maisha yako ,ujasiriamali au unachokifanya kwa ujasiriamali kinatakiwe kiwe ndani yako,kiwe kinaongoza maisha yako,hivyo unatakiwa utambue kwamba unachotengeneza kwa muda huo ni maisha yako ni kifo chako na ni inestment yako pia.

  1. Baada ya kutambua hilo unatakiwa uyaone mafanikio ya investment kwa kipindi cha muda mrefu usitengeneze mafanikio ya muda mfupi,ujasiriamali wako unatakiwa usikuonyeshe chochote kila ukijaribu  kupata picha ya muda mfupi ila ukipiga picha ya muda mrefu unayaona mafanikio hiyo ndiyo aina ya ujasiriamali unayotakiwa kuwa nayo.

  1. Ili kukamailisha mipango ya ujasiriamali wako tengeneza vyanzo shirikishi vya biashara ambavyo vitakuwa na kazi ya kukusaidia kuyafikia malengo makubwa ya ujasiriamali wako. vyanzo hivyo vifanyie utaratibu kama uliotangulia kwenye uzi wa. 

       http://elishachuma.blogspot.com/2013/11/hatua-za-kufuata-unapofikiria-kuanza.html

Comments

Popular posts from this blog

Baadhi ya vitu vinavyosababisha biashara nyingi kufungwa.

Umuhimu na maana ya Logo( Nembo) katika biashara yako.

Aina za malengo na mipango