Jinsi ya kuanzisha biashara bila ya kuwa na mtaji wa pesa.

Imekuwa ni kawaida kwa watu wengi kutambua pesa kama mtaji wa kila kitu katika biashara , lakini katika ulimwengu wa biashara iko tofauti pesa sio mtaji bali pesa ni kiasidizi cha mtaji . Leo nitakupa baadhi ya njia unazoweza kutumia kuanzisha biashara yako bila ya kuwa na mtaji pesa ila kwa kutumia mtaji mbinu na vinginevyo.

Watu wengi  huruka sana sehemu ya kwanza ya mtaji ambayo ndio  chimbuko la mtaji  na kukimbilia kwenye  sehemu zinazofuata na kuendelea bila kujua muhimili wa nyumba ni msingi bila ya msingi mzuri nyumba inaanguka hivyo bila chimbuko zuri la mtaji wako hauwezi kufanikiwa, sasa basi chimbuko hilo ni nini ambalo watu huliruka na kukimbilia mengine.

Kichwa/ akili mtaji wako mkubwa ni kichwa chako na hata wazo na kila kitu kinaratibiwa na kichwa chako mwenyewe ndani ya kichwa ndipo panatengeneza ndoto na ndipo panapofanya ndoto zitimie kwa kushirikiana na viungo vingine vya mwili lakini injini ya mwanadamu ni kichwa katika kufanya mambo ya maamuzi. Kichwa ndio chimbuko la mtaji wako na kila mwanadamu amebarikiwa kupewa kipaji au uwezo wa kufanya kitu fulani ambacho anaweza kufanya bila kufundishwa na mtu, na kupitia hicho kipaji au uwezo unaweza kufanikiwa sana tatizo ni wengi hupuuzia vipaji na uwezo wao binafsi na kuabudu uwezo wa wengine na wengine huona kama vile uwezo wao hautoshi au haujafikia uwezo wa kuanzisha kitu cha kumsaidia.Kipaji chako haufundishwi unazaliwa nacho kuna vipaji ambavyo ni vya wote na kila mtu anakuwa nacho ila asilimia kubwa huwa tunahisi ni lazima uwe hivyo. Huwezi kwenda kutafuta kipaji chako shuleni unaenda shule kuendeleleza kipaji chako. (Mfano wa kipaji cha wote ni kula, kila mtu anapozaliwa huwa anakipaji cha kuchukua mkono kupeleka mdomoni hakuna anaefundishwa hilo ila unaweza kwenda shule kusomea namna ya kula vizuri,kistaarabu na vitu kama hivyo lakini sio kwenda kufundishwa namna ya kula.) nisikutoe sana kwenye mada jitambue unakipaji ambacho kinaweza kuwa mtaji tosha iwapo utakionyesha na watu wakakiona.

Kitu cha muhimu ambacho unatakiwa ukifahamu kwanza ujitambue ili uweze kufuata njia yako na katika lugha za kibiashara kuna kujitambua kwa aina mbili aidha ni mfanyabiasha au mjasiriamali hapoa sasa unatakiwa kujua wewe ni nani na kati ya hivyo viwili unaweza kuegemea sehemu ipi na ukapambana na changamoto zake ukiwa unafurahi kuna msemo fulani husema " Watu masikini huomba matatizo yasiwakute ilhali matajiri huomba matatizo yawakute " hapo wengi mtaanza kujiuliza ni kwa njia gani unaweza kuomba hivyo masikini huchukulia matatizo kama shida hivyo hujitahidi kuyakimbia ili yasimharibie mipango yake ya sasa lakini tajiri huomba matatizo yaje ambapo yeye huona matatizo ni sawa na changamoto hivyo huomba changamoto zimfike ili ajifunze hata itakapokuja kumtokea tena atakuwa anauzoefu tofauti na mwanzo lilipotokea.hivyo ukijitambua wewe ni nani utapita katika changamoto zake huku ukiona njia nyingi za kutokea ni wewe mwenyewe utumie ipi ambapo ni tofauti iwapo umechagua sehemu ambayo sio hapo ili ufanikiwe itakubidi umtafute mtu ambae yeye ndio sehemu yake ili akupe njia na mbinu za kutokea hapo uwezo wako utakuwa umefunikwa na kumuelekea yule anaekusaidia.


Ona kipaji chako kinaruhusu ufanye nini na tumia kipaji chako kama mtaji wa kukuanzishia biashara yako au ujasiriamali wako ambao ndio kipaji chako kitu cha msingi ni kutambua unahitaji watu gani na unawafikia vipi tumia kichwa chako vizuri na akili zako asilimia kubwa ya waliofanikiwa sana au wenye maendeleo makubwa walitumia vipaji vyao kwa umakini ndio wakatengeneza ajira kwa wengine.

itaendelea toleo lijalo......

Comments

Popular posts from this blog

Baadhi ya vitu vinavyosababisha biashara nyingi kufungwa.

Umuhimu na maana ya Logo( Nembo) katika biashara yako.

Aina za malengo na mipango