Jinsi ya kuanzisha biashara bila ya kuwa na mtaji wa pesa. (Sehemu ya pili)

Baada ya kuangalia sehemu ya kwanza wiki iliyopita ya jinsi ya kujiajiri bila kuwa na mtaji pesa leo tunaendelea na sehemu ya pili.
Kama imetokea umeshindwa kugundua kipaji chako bado kuna uwezekano wa kuanzisha biashara yako bila ya kuwa na mtaji pesa haya kitu cha kwanza ni unatakiwa ujitambue wewe ni nani kati ya mfanyabiashara au mjasiriamali halafu ona aina ya biashara ambayo ndani ya uasili wako mwenyewe  ichague kwa umakini halafu andika chini vitu ambavyo unavihitaji ili biashara yako ifanikiwe au ionekane andika pembeni ( Sio mpango biashara)halafu  anza kufanya utafiti wa hivyo vituulivoandika kwa kutafutia mbadala wake sehemu zote ambazo zinahitaji pesa ziorodheshe pembeni halafu anza kutafuta mbinu mbadala kwa kila kimoja usikurupuke chukua muda ili ufanye maamuzi mazuri kama ulichochagua kikondani ya sehemu  yako ya kujitambua kupata njia mbadala sio kazi ngumu.( Safari ya mafanikio huanzia mbali sana hakuna tajiri ambae alianza huku akiwa tajiri au alianza na mtaji mkubwa )anza kufanya na kushughulikia biashara yako kwa ngazi yako usilazimishe ianzie juu. Kama ulichochagua kweli kiko kwenye damu yako kufeli ni kugumu  mfano: Asili ya kabila la wachaga ni biashara hivyo kwa mchaga kuwa mfanyabiashara ni kitu rahisi kuliko msukuma, Mmasai asili yake ni ufugaji ( Mjasiriamali) hivyo kwa huyu kufanya ujasiriamali ni kitu ambacho kiko ndani ya damu yake hivyo ni rahisi kupata mbadala wa changamoto.

Baada ya kupata mbadala wa kila sehemu ya fedha anzisha biashara yako kwa kutumia mibadala hiyo ambayo itakusaidia wewe kukamilisha malengo yako bila ya kugusa pesa yako. Katika biashara kuna mafanikio aina mbili , yanayoonekana na yasiyoonekana   watu wengi huangalia mafaniko yanayoonekana tofauti na yasiyoonekana mafanikio yasiyoonekana ndio mafanikio ya kweli kwani mafanikio ya kuonekana ni matokeo ya mafanikio yasiyoonekana. Na mara nyingi unapoanza biashara yako mafanikio yasiyoonekana ndio mengi kuliko mafanikio yanayoonekana watu wengi huishia hapa pia sababu tu yeye anataka mafanikio yakuonekana au watu alionao wanahitaji mafanikio hayo basi anaamua kuachana na hiyo biashara kwa kuona haina matokeo chanya japo yapo hayo matokeo chanya katika maisha yake mwenyewe. Kama unachokifanya unakifanya kwa moyo mmoja mafanikio yake utayaona kwanza wewe ndio wengine watakuja kuyaona lakini  wewe kwanza. Pia tatizo kubwa wengi wanahitaji kuwa mabilionea ndani ya miaka au muda mchache . Asilimia kubwa ya matajiri ni wajasiriamali ambao waliwekeza katika biashara, biashara ya ujasiriamali ikikubalika sokoni mafanikio yake ni makubwa .

Usiwe na papara ya mafanikio wakati hauna hata mtaji angalia vitu gani unavyoweza vifanya kwa hatua na uwezo wako kwanza acha kufikiria kama waliofanikiwa wakati hata haujafanikiwa bado.chini hapa ni mfano wa mtu mwenye asili ya ufugaji. Anavyoweza kufanya ufugaji bila ya kutumia pesa ila akili na uwezo.

Mfano: Umejiangalia ukagundua ujasiriamali wako ni kufuga kuku, hauna pesa ya banda wala ya kuhudumia hao kuku achilia mbali kuwanunua  kuku wenyewe , kitu cha kufanya kama nilivyosema hapo juu andika vitu vinavyohitaji pesa

  1. Banda 2. Matunzo 3. Kuwanunua kuku wenyewe n.k, ondoka nenda sehemu ambapo wanafuga kuku tengeneza

Tengeneza mazoea na mwenye banda, ongea nae kuhusu mpango wako wa kuwa mfugaji pia na mwambie tatizo lako ni mtaji lakini unataka uingie nae makubaliano halafu atakusaidia. Mwambie utamletea au utamuuzia aidha kuku au mayai trei au kiasi fulani cha kuku na ukifikisha wateja kiasi fulani atakupatia kuku na jogoo mmoja , nenda katafute soko na uza kama mlivyokubaliana na ukishafikisha utapewa hapo tayari mtakuwa mmeshazoeana utamuomba waendelee kukaa hapo kwake hadi utakapowatengenezea banda, akikubali subiri hadi kuku atakapototoa chukua yale mayai baadhi yaache mengine toa kwa kuuza kwa vile tayari unawateja unaweza kupeleka na kuuza ukapata kiasi fulani cha pesa hicho kiasi kitunze kama ni kidogo na anza kutengeneza banda dogo la muda subiri kuku wako atotoe tena fanya vivyo hivyo hadi utakaporidhika unaweza kuwahamisha watoe wapeleke kwenye banda lako na sasa utakuwa tayari unasoko na sehemu ya kuwatunzia matunzo yake pia yatatoka katika mayai na utakao amua kuwauza.

UKIWA UNAFANYA KITU KWA MOYO WOTE HUWEZI KUKOSA MBADALA WA CHANGAMOTO.


Fanyia kazi utambuzi wako na biashara ya moyo wako.UTAFANIKIWA tatizo kubwa kwa sasa ni uwezo wa kutambua ipi ndio njia sahihi ya moyo wako sababu wengi wanatamani vingi .

Comments

Popular posts from this blog

Baadhi ya vitu vinavyosababisha biashara nyingi kufungwa.

Umuhimu na maana ya Logo( Nembo) katika biashara yako.

Aina za malengo na mipango