Kwanini wajasiriamali wengi wanafeli?

Kumekuwa na watu wengi ambao wamekuwa  wanahitaji kuwa wajasiriamali lakini asilimia kubwa wanakuwa ni wale ambao wanakuwa wamefeli mipango mikubwa au kuna kitu kimewasukuma ,vitu ambavyo unatakiwa usifanye kwa kudhani unatengeneza maisha utakuwa unapotea.

  1. Kuna kundi ambalo wao huanza ujasiriamali baada ya kuona umri unaenda au wanategemewa sasa na aidha famili a au kadahali Usifanye ujasiriamali kwa kuona umri umeenda upate kitu cha kujishikiza, hapo utafeli kumekuwa na watu wengi ambao hadi astaafu ndio anaanza ujasiriamali au baada ya kuona umri umeenda ndio anatafuta kitu cha kumpatia ujasiriamali hii ni mbaya na kufanikiwa kwake ni kugumu sana, ujasiriamali sio nyongeza ya ulichonacho ujasiriramali ni msingi wa ulichonacho kama hukutengeneza msingi mwanzo ujue hata uweke ukuta imara kiasi gani dhoruba ikija ni lazima nyumba itapata mtikisiko.

  1. Wapo wengine ambao wanafanya ujasiriamali  baada ya kukosa au kutuma sana maombi ya kazi ukifanya ujasiriamali wa aina hiyo utakuwa unakosea pia ujasiriamali sio njia mbadala wa kazi yako na tatizo kubwa linakuja kujitokeza mtu anapotaka matokeo ya ujasiriamali yawe sawa na ya kazi aliokuwa amepanga kuifanya .

  1. Asilimia kubwa ya wanaofeli ni wale ambao hata elimu ya kujitambua mwenyewe hana, unaweza kuja kumpa wazo la biashara leo kesho yeye akaanza nalo hata bila kuangalia kwa undani kama linaendana nayeye pia bila hata kulinganisha hiyo biashara na yeye wala kufanya utafiti matokeo yake mara nyingi ni kufeli.



Ujasiriamali sio kitu cha kufanyia majaribio au kufanyia maonyesho asilimia kubwa ya watu ambao tunawachukulia mifano na vioo vya ujasiriamali walitumia muda mwingi sana hadi kufika walipo na wengi waliacha mambo yao ya msingi katika maisha ya kawaida  kama masomo, kazi, familia n.k kwa ajili ya kufikia hapo walipo usitafute majibu ya haraka sana katika ujasiriamali wako. UTAFANIKIWA



Comments

Popular posts from this blog

Baadhi ya vitu vinavyosababisha biashara nyingi kufungwa.

Umuhimu na maana ya Logo( Nembo) katika biashara yako.

Aina za malengo na mipango