Kazi na Aina za Branding
Karibu katika muendelezo wa somo la Branding na leo nimekuletea kazi na
aina za Branding katika maisha ya biashara zetu, watu wanafikiri Branding ni kitu kigeni katika ulimwengu wa biashara La Hasha! Branding sio kitu kigeni na kila mtu kila siku anafanya Branding.Hapa chini ni baadhi tu ya kazi za Branding katika biashara yako.
aina za Branding katika maisha ya biashara zetu, watu wanafikiri Branding ni kitu kigeni katika ulimwengu wa biashara La Hasha! Branding sio kitu kigeni na kila mtu kila siku anafanya Branding.Hapa chini ni baadhi tu ya kazi za Branding katika biashara yako.
Branding ndio muongozo au chanzo cha mauzo yako, iwapo utajibrand vibaya mauzo yako yatakuwa mabaya na iwapo utajibrand vizuri mauzo yako yatakuwa mazuri,Kazi ya masoko ni kuipeleka Branding nje ya ofisi ambapo kama ahadi na muonekano ulioweka kwenye brand yako utakuwa mzuri na wenye kumvutia mteja basi huyo atakuwa mteja wako ila ikiwa tofauti na hapo utakuwa umemkosa mteja.
Kazi za Branding
Brand hutambulisha muonekano ,ubora wa kuaminika kwa watu, huku bidhaa za generic
(kawaida) hazijulikani na haziaminiki ,hata hivyo brand ni ghali na
inahitaji mipango ya muda mrefu
Brand hutofautisha
bidhaa na hufanya bidhaa kutambulika mapema
Brand inaruhusu
mtumiaji kutengeneza maamuzi na matumizi ya bidhaa
Brand hutengeneza
thamani halisi kwenye macho ya washirika wa kibiashara na hupenyeza thamani
ndani ya macho ya mtumiaji
Branding hutengeneza
trademark ambayo huongeza thamani ya bidhaa.
Aina za branding.
- Brand kama bidhaa
Hufanya kazi ya
ubora na thamani ya brand.
Katika mkusanyiko wa
matangazo ya bidhaa nyingi, mtumiaji huhitaji kujua jinsi ya kuchagua bidhaa
moja juu ya nyingine, hivyo kwa kulinganisha udhania wake pale anapoamua
kufanya hivyo huwa hana muda mwingi wa kulinganisha ,huamua kuchagua bidhaa
ambayo inakidhi haja zake kutokana na brand.
- Brand kama mfumo/kampuni
Hutengeneza
muonekano chanya wa brand na huonyesha nyuma ya brand kuna mfumo
Uwezo wa ushawishi
wa kampuni hufanya bidhaa kuongeza thamani
- Brand kama mtu
Hii hujishughulisha
na uhusiano na wateja , hutengeneza kukutana kati ya mtu na brand
Ni ngumu kuongeza
soko kama hakuna mahusiano mazuri na wateja wako.
- Brand kama alama
Hutoa muendelezo wa
utambulisho wa brand
Brand inayochukua
akili yako hupata tabia , na brand inayochukua moyo wako hupata kujiapiza
kwanzo.
Karibu katika Semina ya Branding online sehemu ya pili itakayofanyika kupitia mtandao wa Whatsapp kuanzia tarehe 1/05/2015. Jiandikishe kwa kutuma Namba na jina lako kwenda simu namba 0684 047323.ili ujiandikishe sasa. Elimu ya Branding ni ufunguo wa mafanikio ya biashara yako.
Kwa huduma ya ushauri na kufanya Branding ya biashara yako piga namba 0684047323 na utapata maelezo zaidi. ASANTE
karibu
ReplyDelete