Vitu vya kuzingatia unapotaka kuanza au ukiwa mjasiriamali ili ufanikiwe.


Kwanza niwape hongera ambao tayari wameshafanikiwa kupata vitambulisho vya kupigia kura kwa nchi nzima na niwape pole kwa wale ambao bado hawajapata na pia nnawatia moyo kuendelea kuvifuatilia vina maana sana kwa maisha yako naya kizazi chako cha sasa na cha baadae.

Baada ya kutoa salamu hizo sasa nirudi kwenye mada kuu leo hapo juu, taifa letu linapoteza sana nguvu kazi ya taifa katika vitu ambavyo havina mafanikio na malengo chanya kwa maisha ya mhusika na taifa na kutokana na kupunguza umakini katika hilo sasa hivi tumejikuta vijana wengi wanamaliza mafunzo ya elimu zao lakini hawana kazi wanabaki kuwa omba omba na wadandiaji wa kazi wasizokuwa na weledi nazo.

Leo nitaongelea kwa upande wa wajasiriamali wadogo ambao wanafanya biashara ndogo ndogo kwa minajili ya kupata kipato cha kuendesha maisha yao ya kila siku na wale ambao wanafikira kuingia katika ujasiriamali au biashara. Asilimia kubwa sana ya vijana wanafeli katika biashara na ujasiriamali kwa kukosea baadhi ya vitu ambavyo walitakiwa wavifahamu mapema lakini wanajikuta vinawarudisha na nyuma na kufeli. Katika hali ya kawaida unaweza kuona kama hakuna kilichopotea lakini ukiangalia kwa undani utaona umepoteza muda,ufanisi,mali na hata malengo kwa ajili ya kutegemea kitu ambacho haukuwa na malengo nacho.

Baadhi ya vitu hivyo ni pamoja na :-

               1. MUDA

ujasiriamaliAsilimia kubwa sana ya wajasiriamali wadogo wanafeli kutokana na kutokufanya mahesabu ya muda wao na biashara au ujasiriamali wanaoufanya ambapo matokeo yake inakuja kuwa tofauti na malengo sababu kama haujaset muda hauwezi kuwa na malengo thabiti. Wajasiriamali wengi wamekuwa hawana uwekezaji mzuri katika wakati utakuta mtu anaanzisha ujasiriamali kwa ajili ya kujaribu na inamchukua muda mwingi bila ya kuuhesabu matokeo yake umri na malengo vinapishana anajikuta hawezi tena kufanyia kazi malengo mama anaishia kujishikiza shikiza na vijikazi au kibarua ili mradi apate chochote kitu kwa ajili yake au yeye na familia yake. Hivyo unapoamua kufanya ujasiriamali amua kufanya na jifunge kibwebwe kupambana na kila kitu na muda uwe ndio wa msingi kwako hata tunaowaita mifano hai walitumia vizuri muda wao kuna walioacha shule,Chuo,kazi nk lakini unaacha tu pale unapoona muda wako na malengo vinapishana iwapo utaendelea kufanya hiki na kusubirisha malengo yako utakuwa unapoteza muda mwingi lakini usimamizi wa muda ni muhimu.

2.     MALENGO

ujasiriamali
Baada ya kuangalia muda sasa tunakuja pacha wake malengo.Malengo katika biashara au ujasiriamali ni muhimu sana lakini kwa wajisiriamali wadogo wadogo wengi wao huwa hawana malengo ila wana matarajio hawaweki malengo kwa ajili ya ujasiriamali au biashara yao wao wanasubiri matarajio ya biashara yenyewe itakavyokuwa unapofanya biashara au ujasiriamali ni sawa na unaingia vitani hauwezi kuingia vitani unategemea vita itaamua mimi napambana tu, halafu uje ushinde kwa kishindo japo kuna wenye bahati vita ikawa ni nyepesi ukashinda lakini kwa vile ushindi wako ni mwepesi huwezi kupata fundisho kutokana na vita hiyo ni rahisi sana kwa wewe kubweteka na ushindi kwa kujiona unaweza kumbe umekutana na mvua nyepesi siku adui akirudi kwa ajili ya vita utashindwa vibaya .nimeelezea dhana nzima ya kwann uweke malengo katika ujasiriamali au biashara yako mapema sababu biashara ni vita.


3. UJASIRI

ujasiriamali
Ujasiri kama neno ujasiriamali lilivyo unatakiwa ujasiri wa hali ya juu kuwa mjasiriamali au mfanyabiashara hasa unapoanzisha biashara yako ni ngumu sana kufanikiwa mara moja tu unapoanza hivyo ujasiri unatakiwa sana katika kupambana na changamoto za biashara au ujasiriamali na kitu kibaya ambacho huwa kinatokea ni kwamba biashara zinazotengenezwa huwa zinakuwa ziko nje ya weledi wa mhusika mfano dokta atafungua duka la mahitaji ya nyumbani, au aliesomea ualimu anaenda kuwa dreva anakuwa anafaya kama kwa kujishikiza au kwa muda mfupi hivyo ujasiri wako unakuwa unapungua kutokana na akili unavyokuwa umeiaminisha,Ujasiri wako ndio unaokuweka juu kwenye soko uwzo wa kupambanua na kutatua vizuizi ndio unaokusimamisha sokoni hivyo kama mjasiriamali anapungukiwa na ujasiri mwisho wake ni kufeli.


4. MFUMO

ujasiriamali
 Hapa katika mfumo ni sehemu kubwa sana, ambapo mfumo wetu wa kibiashara ndani ya nchi haumpi nafasi sana mjasiriamali mdogo, mfumo wetu wa kibiashara unampa unafuu zaidi mwenye uwezo kubwa hivyo kwa wajasiriamali wadogo ikitokea akaingia sokoni anajikuta mfumo umemtupa mkono lakini hadi agundue kama mfumo umemtupa mkono tayari anakuwa ameshawekeza nguvu na fedha ndani yake, tayari hilo linakuwa ni tatizo.

5.  MAISHA YA KUIGA

ujasiriamaliSasa hivi kumekuwa na wimbi  kubwa la wafanyabiashara wanaojiita wajasiriamali ambapo wanachokifanya ni biashara lakini wanaita ujasiriamali hii inatokana na kuiga mambo, kuna watu ambao huangalia mafanikio ya biashara na kuingia na wao kuanza kuifanya hawa wanafanya biashara kwa kuiga na hili huwapa shida wengi aidha ni kutokana na kukosa wazo zuri la kutumia au kutokana na kukosa muongozo wa biashara anayotaka kuifanya matokeo yake ni kuingia mzima mzima na kuishia hasara katika ulichokifikiria hii imewakuta wengi sana.


6. ELIMU

ujasiriamali
Asilimia kubwa ya wajasiriamali hawana elimu ya ujasiriamali wanakuwa na elimu ya kufikiria hili ni tatizo ndio maana sasa hivi wengine wameona ni mtaji ukiwa na elimu ya kufikiri utaitumia kufikiri kipi ni sawa na kipi sio sawa lakini ukiwa na elimu ya ujasiriamali unakuwa na elimu ya kutambua nifanye nini kwa muda gani na matokeo yake ni nini? Na pia hata kuziona fursa zinapotokea kuliona tatizo kama changamoto kulitatua kijasiriamali “ Mfano, nilisoma katika kitabu Fulani kulikuwa na biashara 3 zinazotoa huduma inayofanana, baada ya biashara kuwa mbaya kwa kipindi kirefu mwenye biashara ya kushoto aliandika punguzo 20% akaanza kupata wateja kwake baada ya muda na yule wa kulia akashusha punguzo 30% wateja wakawa wanaenda na kwake hebu jifikirie ukiwa kama mfanyabiashara wa katikati utafanya nini?.......ambapo alieweka 30% anauza kwa bei ya kurudisha gharama hakuna faida, (Ntasubiri jibu lako kwenye sehemu ya komenti chini ).hivyo unapokosa elimu sahihi kwa kitu sahihi ujue mafanikio yake ni ya kubahatisha sio ya lazima.

Hitimisho.

Kwa leo naishia hapo ushauri wangu kwa wajasiriamali kwanza wanatakiwa wapate elimu ya ujasiriamali ili waweze kuuelewa mfumo wa kibiashara ambao utawapa ujasiri wa kupanga na kusimamia malengo kulingana na muda

Jibu la mfano hapo juu litatoka ndani ya komenti zitakazowekwa hapa chini.Yule mfanyabiashara wa katikati alifanya nini?


Kujiunga na kundi la whatsapp branding tuma namba na jina lako kwenda namba 0684047323 (Whatsapp sms tu), pia unaweza kunipata kwa ukaribu zaidi kwa kuniandikia email(elishachuma@gmail.com) au like page yangu Elisha Chuma.


Comments

Popular posts from this blog

Baadhi ya vitu vinavyosababisha biashara nyingi kufungwa.

Umuhimu na maana ya Logo( Nembo) katika biashara yako.

Aina za malengo na mipango