Kwanini 40 ?
Kwanini vitu vinaangukia siku ya 40 |
Historia,zama na ukweli vinatupeleka mbali sana lakini hii
dhana ya 40 haijatumika kwa mtoto tu vipo vingi leo tutaangalia kwanini 40.
Sasa basi katika ulimwengu war oho kuna kitu kinaitwa Aura hiki
kiko kwenye mwili wa hauwezi kukishika wala kukigusa ni kama tabaka lililopo
juu ya mwili wako ambalo linakusaidia na kukukinga na nguvu za nje,mfano
unaweza kutembea ukahisi mwili umesisimka ghafla tambua hapo aura yako imefanya
kazi,ama umepima na unaumwa lakini hujanywa dawa na unajiona mzima tambua aura
imekuponyesha vipo vingi kuhusiana na hili nisiende ndani sana,mtoto
anapozaliwa aura yake inakuwa haijajitengeneza hivyo zile siku 40 huwa za
kuitengeneza aura na kuifanya ikomae iwe na uwezo wa kupambana na nguvu za
walimwengu,mzunguko huu hutumia siku 40 ndipo inakuwa imekomaa ukimtoa ama
ukimkutanisha na walimwengu kabla ya muda wake inamaana aura yake inaweza
kuathirika sababu itajitengeneza tayari ikiwa na madhaifu, mfano: mtoto akiwa
mchanga kabla ya siku 40 ukimtoa akakutana na watu wa aina mbalimbali wote
hawawezi kuwa sawa kiafya,kiusafi,kimatendo,hata kiimani hivyo ni rahisi kwa
mtu anaembeba mwanao kupenyeza ama kumuambukiza kitu ambacho hawezi kukikataa
sababu aura yake haijakomaa.
Lakini pia kwa mtu anapofariki vile vile Aura huwa bado
imeungana nae na vitu vyake huisha nguvu taratibu taratibu hadi kupotea kabisa
siku ya 40,kuna kesi nyingi za watu kutumia vitu vya marehemu kabla ya siku 40
na wakawa wanamhisi marehemu kwenye vitu vyake,hapo sio hisia za kimawazo
inakuwa ni aura inakuunganisha na roho
ya marehemu hivyo anauwezo wa kuwasiliana nae kihisia lakini kwa vile hautambui
lugha ya rohoni unaweza kuhisi mauza uza,ndio maana hata kugawana vitu huwa ni
baada ya siku 40 ambapo inakuwa tayari aura ya marehemu imeachana na vitu na
kuambatana na roho yake.
Kwa upande wa kiimani 40 inamaanisha “ukomavu” hivyo hata
kwenye biblia Yesu alipofunga siku 40 ilikuwa ni ukomavu wa kuanza kazi ambayo
alikuja kuitimiliza,vivyo hivyo kwa Musa ilikuwa ni ishara ya kuonyesha ukomavu
kwa jambo linalofuata mbele yako kiimani,
kwa wana wa Israel wao iliwabidi miaka 40 sababu ya kufikisha Kaanan kizazi
chenye kumtii Zaidi Mungu kumtambua Mungu wa baba zao ambae amewavusha katika
matatizo mengi hata pale ambapo kibinadamu waliona imefika mwisho
aliwapigania,lakini pia ilikuwa ni ukamilifu wa kufikisha jeshi lenye nguvu Zaidi
na wenye uwezo wa kupambana na maadui ikitokea vita hivyo ili ukamilifu wa ahadi
utimie ilibidi kizazi cha Musa kiondoke ili iingie damu changa yenye ari na
morali ya kufikisha na kukamilisha lengo.
Kupitia ukamilifu huo ndio ikaja na misemo mingine kama siku
za mwizi 40,ikiwa inamaanisha siku yako ya 40 ndio ya ukamilifu wako
utapatikana tu zile 39 utaweza kukimbia ila siku ya ukamilifu wako ikifika ndio
40 yako,Life starts at 40,Menopouse n.k vyote ni kuonyesha ukamilifu tu wa
mwanadamu hata kiakili kimawazo na matendo akifika miaka 40 automatic vitu
vinabadilika ndani yake na nje ikiwa tu ni utimilifu wa 40.
Hii ndio maana ya namba 40 “kamilifu”
Chini hapa ni kwa wazazi na walezi tukumbushane kwa watoto
wetu,utandawazi unatutawala sana tunasahau asili na misingi iliyowekwa.
Sasa wazazi wa siku hizi akimaliza tu kujifungua mtoto yuko
kwenye mtandao,tambua ile ni nafsi changa bado haijawa ana uwezo wa kupambana
kabla ya kukomaa tayari unaipeleka kwenye mapambano na kuna nguvu nyingi zisizo
onekana zinazotafuta nafsi changa kuziharibu, unaweza kutoa nafasi ya kuharibu
maisha yote ya mwanao kwa picha moja uliopandisha akiwa mchanga sababu ya
mahaba yako na ulimwengu kutambua kama umejifungua,mtoto anaweza kupandikizwa
magonjwa aura inakua na magonjwa ambayo sio ya asili ama kupandikizwa kusudi
lisilokuwa la kwake mtoto anakuwa tofauti kabisa na matarajio kila siku
unalalamika afya yake mbovu kumbe imeletwa na kuiruhusu dunia kukutana na mtoto
akiwa bado hajakomaa.
Hakuna mzazi aisiependa mwanae hivyo siwezi kuwakumbusha
kuwapenda,ila tukumbuke sio kila tamaduni tunazoziiga zinamanufaa na zina
madhara ya moja kwa moja madhara yanaweza kuwa yasiyoonekana mara moja akakua
nayo na ukayazoea ukahisi ndivyo alivyo kumbe sababu ilikuwa ni kosa la mwanzo.
tulizingatie hili siku 40 sio nyingi mpe nafasi mwanao kuwa na
afya,nguvu,akili,upeo na kusudi imara aliloandaliwa.MPENDE ZAIDI MWANAO WALIMWENGU
WAPO TU.
Elisha Chuma.
Instagram:@elishachuma
Comments
Post a Comment