Makosa yanayofanywa na wanaotoa elimu ya ujasiriamali
Kuna kitu ambacho
wananchi wanakuwa wanapotea bila kujua kumekuwa na wimbi kubwa la watu
wanaohamasisha na kutoa elimu kuhusu ujasiriamali, Sio wote
Watu hao
wanawasaidia watu,lakini wanaruka sehemu kubwa ambayo inawaumiza sana
Watu wanaoamua
kutumia elimu yao kwa manufaa yao,mfano kuna wale wanaotoa elimu kuhusu
Kutengeneza vitu
kama sabuni,shampoo na vinginevyo,hao hutoa tangazo la kuwafundisha watu mbinu
Za kuwa
mjasiriamali, wao hufundisha namna ya kutengeneza hadi unaelewa halafu
wanakuacha.hilo
Ni kosa kubwa sana
kwa wao kumfundisha mtu kutengeneza kitu kinachofanywa na makampuni makubwa
kama kazi yao halafu ukamfundisha yeye kwa shilingi elfu 30, bila kujua atatoka
hapo atatafuta fedha ya mtaji na mtaji wa kwanza unaweza kuwa ni 50,000 tu hapo
ameshapigia hesabu akiuza anauhakika wa kutengeneza fedha nyingi halafu inakuwa
tofauti.
Kumekuwa na wimbi
kubwa la watu wanaoitwa walimu wa ujasiriamali
wanaofundisha mbinu za ujasiriamali siwapingi wala sikidhani nao
wanafanya kazi nzuri kuwasaidia watanzia kumeza ilhali hawajatafuna, lakini
kuna makosa ambayo nahisi sijuini kutokana na hali ya maisha kutafuta fedha za
kujikimu mwenyewe au hawajui bado sijatambua ni kwanini, wanafanya kazi nzuri
lakini inamakosa makubwa,kupokea elimu ya ujasiriamali ni kitu cha busara na neema sana lakini
kuitumia hiyo elimu ya ujasiriamali ni kazi ngumu kuliko hata kuipata.
Tatizo linalotokea
ni kwamba watu baada ya kuelimishwa kuhusu ujasiriamali , waelimishaji huishia
katika eneo la kutengeneza au kufanya ujasiriamali tu ,hakuna kufanya utafiti
kama unaowafundisha ni wajasiriamali au wafanya biashara ( kupata maelezo zaidi
katika tofauti kati ya mfanyabiashara na mjasiriamali fuatilia matoleo ya
nyuma) hivyo kila mtu hupewa elimu hiyo bila kuwapa mwongozo wa biashara ikoje
na soko lake likoje wao huondoka na kuwaacha hivyo hivyo wakiwa na ujuzi wao
bila maarifa ya soko. Hili ni tatizo linalowapata wafanyabiashara wadogo
waliopata elimu ya ujasiriamali wakijaribu kuangalia njia za kutokea kimaisha
wengi wao huishia kuwa maskini zaidi sababu hata kile kidogo alichokuwa nacho
hakitalipa kulingana na matarajio yake ( kinachofanyika ni sawa na wewe uwe
unachimba madini halafu bahati siku moja
ukapata almasi chafu ukataka kwenda
kuiuza ikiwa chafu vilevile kufika sokoni unataka almasi yako iwe na bei ya juu
pia, lakini ukakuta sokoni kuna wenye almasi nyingi safi na ukubwa kama wako na
wanaziuza kwa bei sawa au chini ya ile bei ya kwako. Kama mteja utanunua almasi
safi na kama muuzaji alamsi yako haitauzika sababu haina kiwango, ndio sawa na
inavyowatokea wafanyabiashara hawa .wao hufundishwa kufanya ujasiriamali baada
ya kufundishwa huachwa ili waitumie elimu ile bila kutambua kama elimu
waliyopewa ni kipande tu wanatakiwa watafute au wapewe kitu kizima hukimbila
kuanza kufanya biashara huku wakiwa
hawajui kama sokoni bidhaa kama hiyo tayari ipo mwisho wake kwa kuwa
hawajajipanga watakuta bidhaa zao haziuziki au hazikidhi malengo kutokana na ubora au hata jina tu , ukiangalia kwa juu
juu unaweza kusema kosa ni la mjasiriamali mwenyewe lakini kosa ni la
mfundishaje ujasiriamali ndio aliempotosha kwanza
- Hali ya maisha ya wafundishwaji
Kutokana
na hali ya ugumu wa maisha wafundishaji hawa hufanya semina zao kwenye wilaya
na na vijijini ili kupata watu wengi na pia hutoa elimu hiyo kwa kiwango kidogo
cha pesa ili wapate watu wengi. Asilimia kubwa ya watu ambao hujitokeza ni wale
wenye kipato cha chini na wengi wao huhisi elimu hiyo ni mkombozi wa maisha
yao.
- Namna ya ufundishaji
Wafundishaji
hawa hufundisha kwa kutumia nyenzo za kisasa na huwa na kipindi maalum cha
kutoa elimu hiyo, hivyo mara nyingi hufatilia zaidi kama kile wanachofundisha
kinaeleweka ama la na sio yule wanaemfundisha wamemuandaa au wanammezesha bila
kutafuta.
- Upatikanaji wa vifaa vya kutumia
Baada
ya kutoa elimu hiyo waelimishaji hao huacha namba za simu na maelekezo ya
sehemu watakapopata bidhaa au vifaa vya kufanyia kazi na kutolea
huduma,asilimia kubwa ya sehemu hizo zinakuwa ni mjini mbali kutoka alipo huyu
anaepewa maelekezo.
- Makosa.
Kosa
linalofanyika kwa watu hawa ni kuwapa elimu ya ujasiriamali peke yake bila
kuwapa elimu inayoenda sambamba na ujasiriamali, elimu ya ujasiriamali haitoshi
peke yake kumfanya mtu awe mjasiriamali tuko katika dunia ya utandawazi mambo
yanatakiwa kuenenda kutokana na soko lilivyo na haitakiwi mfanyabiashara
kufanya biashara kwa kujaribu sababu unachojaribu wenzako wanafanya kwa maisha
yao.
USHAURI:
Kama waelimishaji ni
bora kuongeza kiwango cha ada ya kuipata elimu hiyo lakini wahakikishe wanatoa
kifurushi kizima cha ujasiriamali mfano: ukija kunifundisha ujasiriamali wa
kutengeneza sabuni ya maji, ukanielekeza na namna ya kupambana na washindani,ukanipa
mbinu, ukanielekeza taratibu za kufata
na kufanya ili nipate wateja. Itakuwa umenisaidia sana sababu nikifanya nafanya huku nnajua
ninapambana na watu gani na huku ninajua kabisa naingia kwenye vita sihitaji
kuingia bila kujiandaa.
Comments
Post a Comment