Tahadhari kwa wafanyabiashara na wajasiriamali


Taa ya hatari imeanza  kuwaka kwa wafanyabiashara na wajasiriamali wa Tanzania
Asilimia kubwa ya wafanyabiashara, ( wakubwa na wadogo) wanafanya biashara
Kienyeji na kikubahatisha wanafanya biashara kama mchezo wa bahati nasibu kupata
Kukosa  lakini siku sio nyingi mambo na hali itabadilika na kubadili mfumo wote wa kibiashara
Hapa Tanzania.

Kwa kuanza kwa sasa watanzaia wengi wanapata hamasa na hamu ya kuwa wafanyabiashara
Au wajasiriamali kwa inspiration kutoka nchi za nje, kutoka kwa wajasiriamali wakubwa , kutoka
Kutoka katika vitabu vya waandishi wa nje ambao huelezea hali ya biashara au ujasiriamali kwa
Kiwango na uwezo wa sehemu walipo na kwa mjasiriamali  wa kawaida akisoma au kutumi mbinu zile
Zinaweza msaidia sababu kwa kipindi hicho vitu alivyovisoma sehemu anakovitumia havijulikani hivyo
Hata akikosea au kipatia hakuna atakaetambua,hiyo ndiyo hali iliyokuwepo kwa Tanzania ya zamani lakini
Kwa sasa hali inabadilika tena sana .

Pili Kwa sasa wawekezaji wengi wanashawishika kuingia Tanzania na kuanza kuwekeza na kama nchi ikiwa
Na makampuni mengi ya kigeni hata mfumo wa kibiashara lazima utabadilika sababu asilimia kubwa itakuwa
Ni mfumo mpya wazawa wengi watafeli kwa kuwa itakuwa wameshatengeneza majina lakini kwa mfumo tofauti
Ambao wameukopi bila kutumia sawasawa hivyo watajikuta wanapata hasara kwa kuanza  upya na kuanza kutafuta
Sehemu nyingine  kwa mfano: Zamani ilikuwa ukienda Tra kuchukua TIN namba ilikuwa haihitaji sana uwe na sehemu ya
Biashara kama ni ya biashara, Lakini sasa hivi ili upate TIN ya biashara lazima uwe na sehemu ya biashara na watakukadilia wao kwanza kulingana na gharama zote ulizotumia na makisio ya mauzo kwa mwezi, kwanini basi wamefanya hivi hii ni kwa sababu imeonekana watu wanajichukulia tu TIN bila hata ya kuwa na kazi nazo kwa muda husika mtu anachukua kwa dhamira ya ikitokea inahitajika nitaitumia, Sanjari na habari maelezo pia ukitaka kusajili gazeti lazima waone hadi mfano wa gazeti unalotaka,uthibitisho wa fedha za  kulitoa gazeti angalau mara kumi bila kukosa nakadhalika , Hii ni kwa sababu watu wanafanya biashara kwa kuona faida ukiona mwenzako anapata faida katika biashara yake na wewe unataka ufanye bila kujua alianzaje hadi kufikia kwenye hiyo faida mwisho wake unafeli sababu haujui utaratibu wake Ni kitu ambacho kitu ambacho kitakuja kutokea baadae hata katika usajili wa biashara na makampuni itawabidi ili usajiliwe ni lazima ulete (business plan) wakijiridhisha ndio wanakubali kutoa usajili hii ni kutokana na kuwa na makampuni mengi yanayoanza na kufeli bila kuwa na mbinu thabiti.

Katika biashara kuna vitu ambavyo bado tunavichukulia masihara bila kujua maana na umuhimu wake asilimia kubwa ya wafanyabiashara na wanaotengeneza nembo hawajui umuhimu wa nembo katika biashara yake ikitokea ukamuuliza kwanini nembo yako iko hivyo atakujibu ni kwa sababu kila biashara lazima iwe na nembo,baada ya makampuni mengi ya kigeni kuingia yatatokea mabadiliko hata katika nyanja ya matangazo, leo angalia matangazo yanayotolewa na KFC halafu linganisha na yale yaliyopo pembeni yake.biashara inafanyika kienyeji hata wanaojua wanatawaliwa na wasiojua unakuta signboard ya barabarani tangazo limeandika limejaa vitu biashara inavyomiliki hadi karaha tangazo limechafuka lakini kwa kuwa ni jina linalong'aa kwa wasiojua itauza na kupata wateja.


Mabadiliko yanayokuja yanakuja kwa kasi sana ndio maana sasa hivi hata serikali imeng'ang'ania lebo za TBS hii ni kwa sababu mabadiliko yameanza kuonekana zamani ilikuwa kama unajua kutengeneza kitu ilimradi ni cha Tanzania na kimefungwa vizuri hawakifuatilii lakini sasa hivi baada ya kuwa vingi na hawana uwezo wa kudhibiti kwa haraka wanatoa matanganzo ya watumiaji kutokutumia kama hakuna nembo ya Tbs.kila sekta sasa hivi ndi inaamka kuanza kufanya kazi kwa mtiririko unaotakiwa baada ya kuona kasi ya mabadiliko iko juu na bado tuko mbali , hatari ni kwamba wafanyabiashara hawalijui hilo na hawana hata habari nalo leo hii mfate mfanyabiashara au mjasiriamali muulize kuhusu branding atakwambia anajua ya gari,na hata watoa ushauri wengine  ukiwagusia Branding wanakwambia ni kubwa sana kuifanya kwa Tanzania ni ngumu lakini katika biashara bila kubrand ni sawa na kutembea usiku huku umefumba macho unaweza ukaipatia njia kwa vile umeizoea au unaweza kuikosea kwa vile sio kila siku itakuwa vile vile. South Afrika walileta vurugu na ubaguzi kwa wageni kwa sababu walifanya kazi kienyeji na wageni wakaja kubadilisha mfumo wakajikuta hawapo katika mfumo huo ,ni kitu ambacho nakiona kimeshaanza kutokea hata Tanzania kwa wananchi wengi kuanza kulalamika kukosa kazi na raia wa nchi jirani kupewa kazi, tayari maafa yameanza kuonekana japo wanaogundua ni wachache.


Ushauri:
Kwa wafanyabiashara na wajasiriamali  bado muda upo kidogo wa kuweza kubadilisha  mfumo kwavile hata serikali yenyewe bado haijajitengeneza vizuri angalia biashara yako fuatilia Branding jiangalie uko wapi  katika mzunguko wa branding kisha anza kuenenda na mfumo wa dunia nzima ili mabadiliko yanapofika yakukute umebadilika tayari,biashara ni mchezo lakini unasheria zake hivyo unaweza kushinda kwa njia za panya kama anaecheza haujui mchezo ila huwezi kushinda kwa njia za panya kama unaecheza nae anajua mchezo unatakiwa uchezwe vipi.

Comments

Popular posts from this blog

Baadhi ya vitu vinavyosababisha biashara nyingi kufungwa.

Umuhimu na maana ya Logo( Nembo) katika biashara yako.

Aina za malengo na mipango