Vitu vitano vinavyosimamia biashara yako


Biashara pia inavitu ambavyo kila mtu anatakiwa avifuatilie ili uweze kuimanage, biashara nyingi zinafeli  iwapo moja kati ya vitu hivyo vinapopungua au kukosekana hivyo basi kabla ya kuanzisha au kuanza biashara yako jiaminishe unaweza kusimamia vitu vifuatavyo.

1.Branding
Branding ni muonekano wa biashara yako kwa mteja unaemkusudia, hii ikiwa inamaanisha lazima ujue mteja wako anataka akuonea katika hali gani ili akuamini , mteja wako unataka apate kitu gani kichwani mwake mara tu akiiona alama yako nakadhalika,kuijua elimu hii kutakusaidia sana katika uendeshaji wa biashara yako kwa sababu itakuwa ni rahisi kwako kujua saikolojia ya mteja wako na kuepusha kufanya yasiyo sawa katika biashara  na pia ukiiifahamu branding itakufundisha pia  njia za  kupambana na wateja na mbinu za kiushindani.

2.Masoko ( Marketing)
Masoko ni sehemu ambayo inahitaji umakini mkubwa baada ya kufanya brand ya biashara yako kitu kinachofuata ni kutengeneza na kutafuta masoko ya brand hiyo kwa kuwa utakuwa unambinu za kutosha hivyo na ukifahamu vizuri kutafuta masoko biashara yako itakuwa ni brand inayojitofautisha zingine kwa sababu hata kama kukiwa na watu wengi waliofanya brand kila mtu atafanya kwa mbinu zake ili asifanane na mwenzake , hivyo kuijua elimu ya masoko ni jambo la muhimu sana na la msingi katika biashara yako.


3.Huduma kwa wateja(customer care)
Hili ni janga kubwa kwa hapa nchini sehemu kubwa na biashara nyingi hazitoi huduma kwa wateja inayotakiwa na kutokana na kuzoea hivyo imefikia hatua imeonekana ni kawaida kwa mtoa huduma kwa wateja kuto kukidhi haja za mteja na mteja kuondoka kajilazimisha kuridhika wewe mwenyewe ni shahidi katika hili,lakini elimu hii ni ya muhimu sana kwa ukuaji wa biashara yako ili biashara yako ikue katika kiwango unachokihitaji basi inatakiwa watoa huduma wawe na uelewa mkubwa wa utoaji huduma kwa wateja ,kugundua saikolojia ya mteja anapoingia tu ndani ya biashara yako ni faida kubwa kuliko kutomgundua hadi akufanye umgundue.

4.Imani (Believeness)
Imani inasehemu kubwa sana katika mafanikio ya biashara yako na imani yako inachangia kwa kiasi kikubwa aidha kupata au kukosa katika mzunguko wa biashara yako,kila mtu anaimani haijalishi ni ya dini au ya mizimu lakini kila mtu ana imani na imani hiyo huwa ni kwa Mungu wake ambaye huwa anaamini anauwezo wa kumtendea miujiza na kumsaidia haijalishi ni yupi, hivyo basi biashara haihitaji mchanyanyiko wa imani zaidi ya moja ndani yake inahitaji  imani moja tu ambayo itaisimamia siku zote kwa mfano ukiwa unaamini dini halafu ukaenda kwa mganga kutafuta dawa ya kukuongezea wateja biashara yako haitafanikiwa lakini ukiwa haumini dini yoyote tofauti na kwa waganga biashara yako itafanikiwa ndio maana mnaweza wote kwenda kanisani mnaumwa mwenzako akapokea uponyaji na wewe ukakosa au mnaweza kwenda wote kwa mganga mwenzako akapandishwa cheo wewe ukabaki hii ni kutokana na imani yako inakuwa pande mbili Mungu yule yule unaemuomba ili akulinde usiku kucha ndio Mungu yule yule mwizi anamuomba akuibie bila kudhurika na anakuibia bila kudhurika kwanini , hii ni kwa sababu mwizi imani yake iko juu kuliko ya kwako uwezeakano unahirizi na biblia au Quran kwa wakati mmoja. Hivyo imani yako inanafasi kubwa katika biashara yako.

5.Sheria za pesa( Money principles)
Kila kitu kinasheria zake hata kula pia kunasheria zake hivyo hata kwa pesa tunazotumia nazo pia zinasheria zake ambazo kwa kila mtumiaji anatakiwa azitumie ili aendelee kuwa nazo na sheria  hizo hazijalishi ni kwa mwenye pesa nyingi au kidogo ndio maana unaweza kukuta mtu anaelipwa mshahara mdogo anamaendeleo kuliko anaelipwa mshahara mkubwa, hii inamaanisha sheria za pesa ni za muhimu kufuatwa katika kitu chochote sanjari na biashara pia mfano: Pesa iko katika mchezo wa kunyang'anyana kama ikitoka kwako inakuja kwangu na kama ikitoka kwangu basi inakuja kwako, hivyo ili biashara yako ikue na iendelee lazima iwe ndani ya sheria hizo za pesa.

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

Baadhi ya vitu vinavyosababisha biashara nyingi kufungwa.

Umuhimu na maana ya Logo( Nembo) katika biashara yako.

Aina za malengo na mipango