Aina tatu za imani zitakazokurudisha nyuma katika biashara yako


Biashara haiangalii unaamini kupitia nini,  biashara haiangalii wewe ni mkristo,mpagani muislamu au mhindu,lakini kuna imani ambazo biashara inakutengenezea na inataka ufanikiwe kupitia hizo, hivyo ilikufanikiwa katika biashara yako unatakiwa upitie ukipishana nazo lazima matokeo yake hayatakuwa mazuri.

1.Naweza kufanya kila kitu mwenyewe.

 Hii inakuja  pale mtu anapoanza kujiona yeye ni mzuri na mwelevu wa kila kazi katika biashara yake , lakini ukweli ni hauwezi kufanya kazi zote , ufagie , uhasibu,afisa utumisishi, afisa rasilimali watu na hata masoko wewe mwenyewe?
Ukweli ni kwamba hauwezi ukawa mzuri wa hizo kazi zote ni lazima utakuwa na sehemu yako ambayo unaweza kufanya vizuri zaidi ya nyingine ,  na kama unataka biashara yako ifanikiwe fanya anbacho biashara inataka tumia au fanya ambacho unaweza kukifanya vizuri zaidi usilazimishe kwa kutaka kuonekana unajua sana au unaweza kufanya kuliko wengine ila fanya kwa kuangalia ni kipi unaweza kukifanya vizuri zaidi ya vingine na kazi nyingine waachie wengine wafanye kwa upande wao kila mtu afanye kazi ambayo anaiweza na anaimudu ipasavyo na biashara itafanikiwe usiwe mchoyo wa kazi au nafasi sababu ya kufikiria unapunguza faida, faida inakuja katika ufanisi wa kazi na utendaji wa kazi unaweza kuwa ndio unafanya kazi mbili kwa ufanisi na ufasaha lakini kila kazi ikikuhitaji kwa wakati mmoja utafanyaje?

 Njia yako kubwa ya kuongeza mafanikio iko wapi?
Kuna wafanyabiashara wanafanya kazi bila hata kujua ni biashara ipi inawapa nafasi katika soko la ushindani na mafanikio ya biashar a zao, wao wanachojua ni kifanya kazi na kupata kiasi na kukichanganya basi wanaendelea na maisha lakini iwapo unataka biashara yako igfanikiwe kwa kiwango unachohitaji basi hakikisha unatambua vitu kama hizi  ni muhimu sana kwako na biashara yako tambua upenyo wako wa kupitia na njia za kuupitishia huo upenyo na mbinu zake .

Utajisikiaje iwapo utakuwa na uwezo wa kuongeza wateja wako kwa asilimia 20% kupitia mtandao wa kijamii na internet,Vipi kama unaweza kutengeneza bidhaa au huduma mpya ambayo utakuwa na uwezo wa kuongeza bei kwa 15% zaidi? Ni vipi kama unauwezo wa kuongeza bei zako kwa 20%  bila kupoteza wateja wako?

Kukua na kuongezeka kwa uhitaji wako unachangiwa na nini? Maongezi?,Masoko?,Bei? Au kitu kingine?
Zifuatazo ndio hatua za kutambua na kuyafuata mafaniko  makubwa
  1. Tafuta ni sehemu gani inayotoa nafasi ya kukua na kuongeza kwa biashara yako ?
  1. Angalia kama unaweza kutumia hiyo nafasi kwa mafanikio ya biashara yako au unahitaji mkufunzi kuja kukusaidi a kukuonyesha njia na kuwahisha,kurahisisha  na kuifanya njia ya mafanikio zaidi
  2. Fanya kitu kuhusiana  na hilo .

Watu wengi huogopa kwenda kwa wataalam na washauri kwa kuhofia gharama na uhakika wa huduma watakayoipata japo ni kweli wapo washauri na watoa huduma ghali sana lakini nakupa siri hakuna alighali halafu hana huduma ya watu wasio na uwezo wa kumlipa nenda mfate atakusaidia kwa uwezo wako usiogope , usijihisi unajua kila kitu jifunze kupitia wakufunzi na pia watafuta pale iakapokuwa ni msaada kwa ajili ya biashara yako.


2.Ili kufanikiwa nahitaji (hakuna) katika biashara yangu 

 

Endelea kujifunza vitu vipya kila siku , fanya kazi mara nyingi uwezavyo  ili ufikie malengo yako , mafanikio ya biashara hayaji kama  hauyatafuti tena sio kuyatafuta tu ni kuyatafuta kwa bidii, na sio kuyatafuta kwa kutapatapa unatakiwa kuwa na biashara ambayo utaifanya kwa muda wako na moyo wako wote ndio hiyo itakayo kufanikisha unatakiwa hiyo biashara kuisukuma na kuisukuma hadi inatengeneza msingi wake . Hivyo hutakiwi kujiamini na kusema eti hauhitaji chochote katika biashara yako ili ufanikiwe ukiwa unamaanisha vya kukufanya ufanikiwe vyote unavyo huo ni uongo na sio kwamba hauna kitu kilichopungua katika biashara yako ila ni kwamba haujui biashara yako,japo biashara ni yako lakini haujui misingi yake  na anfasi yake katika soko ila unaangalia ni imeingiza kiasi gani yaani wewe ni sawa na yule mtu anaetoa 10000/= kufanya kazi ya malipo ya 15 na kufanya matumizi ya 16,000 na mwisho akasema biashara imemlipa kwa vile tu pesa aliyotumia ni 10,000/= aliyoitoa . Urudie sana na kuusoma huo mfano hapo juu na jifunze kutenga kati ya faida na mtaji. Usijiaminishe sana labda kuna vingi ambavyo huvifahamu ila kwa vile haujifunzi ndio maana huvioni jifunze na kujifunza sana utafanikiwa , na utaona biashara haikamiliki siku zote kwa sababu kuna washindani, maendeleo , kufeli au kufanikiwa hivyo vyote ni vitu ambavyo vinasimamia biashara yako.

 

3.Kung'angania mpango mmoja

Hapa naomba nieleweke vizuri ninapomaanisha kukaa na mpango  mmoja si maanishi biashara moja, kuna watu wanaweza kuchanganya pale ninaposema mpango na biashara hautakiwi kubadili biashara lakini unatakiwa kubadilisha mipango , kuna wafanyabiashara na wajasiriamali ambao wao muda wote wa biashara zao wanatumia mpanfgo mmoja tu , ndio tunatakiwa kuwa na mipango  ya muda mrefu katika biashara  lakini haimaanishi hiyo mipango ndio biashara kwamba haitakiwi kubadilika fanya biashara kwa kuangalia na mabadiliko ya nyakati sio  kufanya tu kwa vile ni biashara na umeshaambiwa  inatakiwa iwe hivyo basi na wewe unafanya hivyo hivyo tu muda wote ni lazima uwe na kipimo chake, biashara inahitaji vitu vingi ili ikupe mafanikio yanayotakiwa moja wapo ni kuitambua na kwenda na wakati unatakiwa kwenda na wakati katika biashara yako na sio kwenda na mpango ambao unaweza kubadilika muda wowote .Mipango ni kianzio cha jinsi biashara yako itakavyokuwa , using'anganie mpango wako kwa vile tu ni mpango ambao umejiwekea unatakiwa kuwa ni mpango ambao unaendana na hali ya soko na maendeleo yake.

Comments

  1. Asante kaka kwa elimu yako tunazidi kuelimika na kupata mwanga zaidi kuhusu ujasiriamali na biashara, je nawezaje kupata machapisho yako kwa njia ya hardcopy

    ReplyDelete
  2. asante sana mkuu nashukuru kwa kupata taarifa kama elimu ninayoitoa inakusaidia na upande wa machapisho katika makaratasi kwa sasa bado sijafikiria japo nimeshapokea maombi niko katika mchakato huo nitakapokuwa tayari nitawajulisha kupitia hapa hapa katika blogu yetu pendwa

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

Baadhi ya vitu vinavyosababisha biashara nyingi kufungwa.

Umuhimu na maana ya Logo( Nembo) katika biashara yako.

Aina za malengo na mipango