Vitu vinavyorudisha nyuma wajasiriamali/ wafanyabiashara (sehemu ya 2)

Toleo lililopita nilitoa maelezo kuhusu vitu ambavyo vinarudisha nyuma wajasiriamali wengi na wafanyabiashara, ambavyo ni vitu vya kawaida na vinafanyika na vingine hufanyika kimakosa bila hata kujua.

Unapokuwa mjasiriamali / mfanyabiashara kufeli ni moja ya hatua za ukuaji wa biashara yako hivyo tegemea kufeli kila unapotaka kukuza biashara yako,na kama kuna kufeli ambako ni lazima upitie basi lazima kuwe na namna ya kukabiliana na kufeli huku inatakiwa kila mpango unaoutengeneza uwe na mpango msaidizi wa iwapo utafeli basi huu utachukua nafasi au iwapo mambo yataenda mrama kwa upande huu nitafanya hivi au vile sio kufanya tu huku unawaza na kusema MUNGU atasaidia. Na madhara yote hutegemea  vitu 4 ambavyo ndio vinakuongoza katika biashara yako

  1. Mipango biashara yako( Business plan)

Baadhi ya vitu ambavyo huwa vinawafelisha wengi ni pamoja na jinsi ya utengenezaji au ufanyaji wake, japokuwa mpango biashara ndio nguzo ya biashara wengi hufikiria ni ufujaji wa pesa  na hii ni kwa sababu kitakacho toka ndani ya mpango bishara hakina uhakika na huwezi kukipa uhakika asilimia 100 tofauti na mawazo yake ambayo ameshajiaminisha kupitia hayo.

Katika hili kwa wajasiriamali wengi wadogo na wa kati hutengeneza mipango biashara ya kienyeji na asilimia kubwa huishia kufeli kwa sababu inakuwa haijakidhi ule uwezo unaotakiwa, na baadhi ya vitu ambavyo huwafelisha ni pamoja na ufanyaji wake asilimia kubwa hufeli kwa kushindwa kuelewa mpango biashara unafanywaje na unatakiwa kuwa vipi hivyo hufanya kwa namna na jinsi vichwa vyao vinavyowaambia ambapo wengi hukosea, pia hutengeneza bila kutambua aina za mipango wanayotengeneza utakuta mjasiriamali mdogo ametengeneza mpango biashara wake na kitu kikubwa alichokiweka ni mpango wa mafanikio ndani ya miezi miwili ambapo ataonyesha mathalani biashara yake ni ya kutengeneza vitumbua basi atafanya mara ya kwanza atauza vitumbua kama mama wa jirani yake ambapo atafanya kupunguza kidogo pesa ya mauzo ili siku ikizidi au kupungua inaweza kuendana na mpango wake halafu anapiga mahesabu kwa mwezi anajua atakuwa  na kiasi gani na baada  ya hapo anaangalia faida atakayoipata basi kamaliza mpango biashara wake, hapo unajitengenezea mipango feki ya biashara yako sababu umetengeneza mpango biashara ambao haujakidhi matakwa ya biashara hiyo, ninapokea maombi mengi ya watu kuwatengenezea mpango biashara lakini wengi wao huniambia tayari wakiwa na  biashara hapo inamaanisha tayari ulikuwa na mpango biashara lakini haujakulipa ndio maana unatafuta ambao ni wa kitaalamu, kujitengenezea mpango biashara mwenyewe bila kuwa na weledi nao ni kuiweka biashara yako kwenye hatari ya kushindwa, kitu kingine kinachowarudisha nyuma katika hili ni pamoja na muda wa mpango kutumika asilimia kubwa ya wajasiriamali hutengeneza mpango biashara mmoja tu ambao hauna muda maalumu na wengi huuweka kulingana na soko litakavyoamua kama soko likiukataa basi anaauacha au anabadilisha biashara  tatizo la mwisho kwa upande huu ni kukosea kutengeneza mpango biashara utakuta mjasiriamali au mfanyabiashara katengeneza mpango biashara ambao hauendani na biashara yake anabiashara ya kutengeneza sabuni anafikiria kutengeneza mpango biashara sawa na wa kampuni ya kutengeneza sabuni ambao wanaifanya hiyo biashara kwa kipindi kirefu hilo ni kosa kubwa ambalo linaweza kurudisha nyuma na kuifanya biashara yako ishindwe.

Suruhisho: Tafuta watu maalum wenye weledi wa kutengeneza mpango biashara waeleze kuhusu biashara yako na watakutengenezea kulingana na hali yako, uwezo na soko lako pia ambapo utapata faida ya vingi sio tu mpango bali hata mchanganuo wa biashara yako kitaalamu, usiogope kuwafuata kwa kuhisi ni gharama kubwa hata wanaochaji gharama kubwa wana nafasi gharama ndogo. Kupata maelekezo zaidi kuhusu jinsi ya kutengeneza mpango biashara fuatilia kwa kubofya HAPA na HAPA

  1. Muundo wa biashara yako .

Hapa pia kunatatizo kubwa ambalo wengi hufikiria na kukumbuka shuka kukiwa kumekucha wengi wanapenda kufanya biashara au ujasiriamali lakini hawako tayari kufuata taratibu za kisheria  kutengeneza biashara hiyo  asilimia kubwa hawafuati sheria na taratibu za kufanya biashara hiyo na kwa sababu katika mpango wa biashara zao hakuna sehemu hiyo hivyo hufikiria kwanza vitu vinavyohusiana na ofisi zao bila kufikiria serikali pia inautaratibu  na mwisho wa siku utaona inakuwa shida kwao tena kufukuzana na sheria au hata kufunga biashara zao au kupigwa faini kubwa, hili linawarudisha nyuma wengi japo  wapo ambao hawajui hata hatua za kufuata ili kuzihalalisha biashara zao, muundo wa usimamizi na utendaji kazi pia ukiwa ni mbovu lazima biashara itayumba hakuna kitu kisichokuwa na heshima au adabu katika utendaji kazi wake hata unapokula chakula au kutembea kuna vitu ambavyo ni lazima utavifanya kwa sababu ndio adabu na heshima ya unachokifanya vivyo hivyo na kwenye biashara pia,  na kitu cha mwisho ni muundo wa mbinu za biashara yako kuna watu ambao kazi yao ni kukopi na kupesti ( kurudia kila kitu kama mtu mwingine) yaani amepata wazo la  biashara kwa kukopi kwa mtu pia mbinu pia atataka kutumia zile zile kwa kuwa biashara ni ile ile, haitakiwi iwe hivyo ni lazima mbinu zako zikutofautishe na zikutenge nawengine.

Suruhisho: Fuata taratibu za kisheria kabla ya kuanza biashara yoyote tambua hatua zake za kuianzisha kisheria wazo lipo tu na wateja watakuwepo tu aidha ukifata sheria au usipofuata ila usipofuata ni usumbufu na hasara ambayo unajitunzia. Hivyo fuata taratibu zote za kisheria ili kuihalalisha biashara yako.


  1. Kiwango cha bima yako

Hapa kuna tatizo kubwa kwa hapa nchini hata bima za magari kwa sasa watu wanakata kwa kuwa tu ni lazima lakini watu hawapendi na hawajui bima inafaida gani na inawasaidia nini, Bima ni muhimili wako kipindi cha majanga hebu fikiria unapopata janga na ndio umewekeza kila kitu chako katika biashara yako ukiwa huna bima yoyote ni kwamba ndoto na mafanikio yako yote yamefukiwa na janga lakini hebu fikiria upande wa pili iwapo ukiwa na bima ambayo itakuwezesha kulipwa na kurudishiwa vitu vyako kama zamani ni kiasi unakuwa unfanya kazi na biashara yako kwa kujiamini, tunafurahia tu kusikia kuna watu wamekatia bima hadi miguu yao hiyo ni kwa sababu majanga ni moja kati ya vitu ambavyo vitakukuta hivyo jiandae kwa hilo kuna usemi unasema usipojiandaa kushinda basi jiandae kushindwa , Bima ni kitu cha muhimu kwa maisha yako na biashara yako. Kampuni zipo nyingi tu zinazohusika na hilo bima zipo nyingi na zina faida kubwa kwako na biashara yako.

Suruhisho: Epuka hasara za majanga kwa kuiwekea bima biashara yako.

  1. Kusaini mikataba 

Hili pia ni moja kati ya sababu zinazowarudisha nyuma wajasiliamali wadogo , asilimia kubwa huogopa tarakimu za pesa bila kuangalia gharama husika hivyo kujikuta wanafanya kazi kubwa kwa malipo kidogo, pia wapo ambao husaini mikataba kutokana na shinikizo tu aidha hana fedha au biashara haiendi sawa, wapo ambao wao huangalia faida za muda mfupi na kukurupukia na asilimia kubwa huwa ni kutokuwa makini na hivyo husaini bila hata kujua wanakubali na kuingia mkataba wa aina gani.



Suruhisho: Kuongeza umakini katika mikataba unayosaini usichoke kusoma kwa kuwa tu umepewa baadhi ya faida au madhumuni yake bila kusoma angalia mkataba unaoingia unafaida gani na unakupa uhuru na madhara gani kabla ya kusaini.

Comments

Popular posts from this blog

Baadhi ya vitu vinavyosababisha biashara nyingi kufungwa.

Umuhimu na maana ya Logo( Nembo) katika biashara yako.

Aina za malengo na mipango