Mambo yanayorudisha nyuma wajasiriamali/Wafanyabiashara

Kuna mambo mengi ambayo wajasiriamali wengi huyaangalia kama hayana nafasi sana  wanapoanza ujasiriamali lakini baada ya muda na mambo kugeuka ndipo hukumbuka umuhimu wake, na mengi kati ya hayo huwa yanakataliwa na misemo ya mitaani ambayo huwa inaathari za moja kwa moja au vinginevyo kwa mfano maranyingi unapoamua kufanya kitu huwa unafuta mawazo yote ya kufeli ingawa katika hali halisi kufeli kupo katika hilo hilo unalolifanya na wengi huwa wanatumia msemo wa " unapofanya jambo fanya kwa moyo wote usiwaze kufeli sababu utapunguza ari" uwezekano ni ukweli ukiwaza kufeli unapunguza ari ya kulifanya jambo lakini Je unalolifanya linakufeli au halina? Na je ukifikiria kufeli unapunguza ari kwa kuliogopa jambo au kwa kuchukua tahadhari iwapo utafeli? .vivyo hivyo na kwa wajasiriamali wengi pia huwa hawawazi kufeli katika wanachokifanya ni kushinda tu muda wote lakini ukiangalia ukweli ni kwamba hata katika maisha yao ya kawaida mipango yao sio yote inayofanikiwa. Utakuta baada ya mjasiriamali au mfanyabiashara kupewa elimu ya kitu fulani hufikiria kile kitu peke yake bila  ya kuangalia vingine mfano: kwa mjasiriamali/mfanyabiashara aliefundishwa kutengeneza sabuni ya unga anapohakikisha anaweza kutengeneza ile sabuni bila ya msaada wa mkufunzi basi huamua kuanza ile kazi kwa mawazo ya kuifanya iwe ndio biashara yake ya kumpatia kipato na katika  mawazo yake utakuta ni

 

Mtaji: hela aliyokuwa anatunza  kidogo kidogo kwa ajili ya dharura/ mkopo au Mshahara wake
Vifaa: atanunua vichache vya kutosha hela yake kwanza
Kutengeneza: ujuzi anao mwenyewe hivyo haina gharama
Wateja: majirani wake eneo analo ishi na wenye maduka ya karibu na yeye na ndugu zake kwanza
Mpango endelevu: akishauza akapata faida ataongeza kiwango cha uzalishaji

Kwa mjasiriamali huyu kama unavyoona hapo juu hakuna sehemu ya kufeli, lakini je  ni kweli anachokifanya kitafanikiwa ? Hebu fikiria kwa mfanyabiashara kama huyu hayo ndio mawazo yake na mpango wake kwa biashara anayoifikiria kuletea kipato je ameangalia na uwezekano wa kufeli katika anachokifanya hebu fikiria ni athari gani atazipata iwapo Serikali itakataza kutumia sabuni ambazo hazijasajiliwa sehemu husika? Itakuaje iwapo vitendea kazi vitakuwa vichache kulingana na mpangilio wake? Itakuaje iwapo majirani na ndugu hawatamuunga mkono kwa kununua bidhaa yake, itakuaje siku ya kumaliza kutengeneza sabuni yake mvua ikanyesha ikanyeshea sabuni zote na ni sabuni za unga? Itakuaje iwapo gharama za utengenezaji zitapishana na gharama za mauzo? Jibu la maswali yote hapo juu ni moja KUFELI inatakiwa kuchukua tahadhari zote kabla ya kuanza kitu chochote ndio maana hata katika mipango kuna mipango ya muda mrefu na muda mfupi yote hii ni kuchukua tahadhari za jinsi ya kufikia malengo ya mpango mkuu .

Unapokuwa mjasiriamali / mfanyabiashara kufeli ni moja ya hatua za ukuaji wa biashara yako hivyo tegemea kufeli kila unapotaka kukuza biashara yako,na kama kuna kufeli ambako ni lazima upitie basi lazima kuwe na namna ya kukabiliana na kufeli huku inatakiwa kila mpango unaoutengeneza uwe na mpango msaidizi wa iwapo utafeli basi huu utachukua nafasi au iwapo mambo yataenda mrama kwa upande huu nitafanya hivi au vile sio kufanya tu huku unawaza na kusema MUNGU atasaidia. Na madhara yote hutegemea  vitu 3 ambavyo ndio vinakuongoza katika biashara yako


  1. Mipango biashara yako
  2. Muundo wa biashara yako
  3. Kiwango cha Bima yako
  4. Mikataba unayosaini


Hivi ndivyo vinavyochangia kufeli kwa biashara yako iwapo utaviweka vizuri na kuvisimamia kwa uhakika basi biashara yako itasimama na kuendelea siku zote, toleo lijalo nitavielezea hivyo vitu vinne hapo juu kwa undani unakose wapi na unatakiwa ufanye nini. Mungu akutangulie tukutane tena toleo lijalo, kwa maswali na muongozo wa mada hii andika maoni maswali au hoja kupitia eneo la comment hapo chini au tuma email moja kwa moja elishachuma@gmail.com

Comments

Popular posts from this blog

Baadhi ya vitu vinavyosababisha biashara nyingi kufungwa.

Umuhimu na maana ya Logo( Nembo) katika biashara yako.

Aina za malengo na mipango