Muendelezo wa umuhimu wa Logo katika biashara yako
Kukutambulisha katika soko
Logo
yako ndio inayokutambulisha katika soko la ushindani ,soko la biashara na hata kwa wateja hivyo logo yako inatakiwa
iwe ambayo ni maalum kweli ili utambulisho wako usije kuwa na muonekano mbaya
au usiovutia logo yako ndio ambayo inatathminiwa ndani ya soko mtu anapoiona
logo yako ndio anakutambua.
Logo ni muongozi wa biashara yako
kwa sababu unapokutana na mteja ananunua kitu
kutokana na utambulisho na muendelezo wa logo ya bidhaa unayotengeneza siku sio
nyingi nilipokea simu kutoka kwa mtu nisiemfahamu akawa anataka nimtengenezee
logo kawaida yangu huwa ni kupata maelezo nikamuuliza ameipatia wapi namba
yangu na aina ya logo anayotaka alishangaa kidogo kuona nakuwa na maswali
kumzidi lakini alielewa na kitu alichokuja kunijibu ni aliona business card
yangu kwa mtu akawa amependa logo yangu ikawa imemvutia kiasi kwamba akawa
anataka nayeye nimtengenezee nyingine
lakini iwe jamii ya hiyo ya kwangu, hivyo logo yako ni muongozo wa biashara
sababu ndio kitu anachokutana nacho mteja kabla ya kukutana na wewe.
Kukutambulisha uepo wako.
Logo
inatambulisha uepo wako katika kila kitu nembo inachukua nafasi kubwa ya
kukutambulisha kuliko hata binadamu nembo unauwezo wa kuiweka sehemu na
ikakutambulisha kwa kila anaeiangalia na siku hizi maana ya logo sio kuelezea
shughuli unayoifanya ila nembo sasa hivi inachokifanya ni kukumbusha tu na uepo
wa biashara miliki ya nembo hiyo ambapo wewe mwenyewe ndio utakaekumbuka ni
huduma gani au bidhaa gani unayoihitaji kutoka kwa mmiliki wake mfano:
nilimuuliza kuna mtu alikuwa anafanya kazi kampuni ya mawasiliano nikamuuliza kwanini huwa
wanatumia pesa nyingi kuweka matangazo barabarani lakini wanaweka jina la kampuni na nembo yao
peke yao hakuwa na majibu ya kueleweka na mwisho alinijibu hajui , lakini maana
ya kufanya hivyo hiyo ni kutokana kampuni inatoa huduma zaidi ya moja hivyo
iwapo wataandika ni tangazo la kitu kimoja au kwa ajili ya kitu kimoja basi
watakuwa wamefungia uwezekano na upenyo kwa huduma nyingine ambazo zinatolewa na kampuni hiyo hiyo.
Kukuza biashara yako
Logo
inatumika kukuza biashara yako sababu ndio alama ambayo inakutambulisha katika
sehemu zote unazohitajika kuonekana wewe na biashara yako , biashara yako
inasubiri nembo itoe utambulisho ndio yenyewe ifanye kazi, hivyo ukuaji wa
biashara yako uko mikononi mwa nembo yako ikishirikiana na vingine lakini cha
kwanza katika ukuaji wake ni nembo.biashara yako itakua iwapo logo yako
itasambaa na kuonekana sehemu nyingi.
Kuongeza ufanisi wa kazi
Logo
inaongeza ufanisi na muonekano wa kazi
yako iwapo utaitumia vizuri logo ukiiweka katika kila sehemu ambayo unatakiwa
uonekane itakuongezea ufanisi na muonekano wa biashara yako kupitia yenyewe
logo inakuwa kama jaji wa jinsi ya ufanyaji kazi wako kama logo yako
haijapangiliwa na hainamuonekano mzuri na vitu kama hizo lazima itakupunguzia
muonekano wako hata kama ufanisi ni mzuri logo ndio inayotoa muongozo wako .
Toleo lijalo nitaeleza logo inatakiwa iweje na uifanyeje ili iendane na wakati pamoja na soko linavyohitaji
Toleo lijalo nitaeleza logo inatakiwa iweje na uifanyeje ili iendane na wakati pamoja na soko linavyohitaji
Comments
Post a Comment