Vitu ambavyo vinatakiwa vionekane kwenye nembo yako
- Iwe ya
kipekee
Watu wengi wamezoea
kuwa wanatengeneza logo kwa kuigilizia ya sehemu fulani au kwa kufuatisha mfumo
wa kampuni fulani , wengine hufanya kama logo nyingine kisa tu ni kwa vile
imempendezea machoni kwake au ameipenda bila kujali ujumbe utakaotoka baada ya hapo,
nembo yako mara zote inatakiwa iwe ya
kipekee na isifanane na nembo yoyote dunia nzima. Hasa katika soko ulilopo,
unatakiwa kuifuata maana halisi ya nembo kama nembo ni utambulisho wako iweje
uwe unafanana na utambulisho wa mwingine na iwapo umeigilizia kutoka kwa
mwenzako inamaanisha tayari yeye brand yake ni kubwa kuliko yako hivyo
ukitengeneza nembo inayofanana nayakwake ni kama vile unamsaidia kumkumbushia
watu na kumtengenezea nafasi katika vichwa vya wateja wake. Mfano: leo hii
ukipita sehemu ukaona nembo inayofanana na ile nembo ya brand ya cocacola
utamkumbuka nini brand ya cocacola au brand ya yule aliyeitengeneza . Ukweli ni
kwamba utaikumbuka cocacola na unaweza hata kuanza kujiuliza kama wamebadilisha
nembo utabaki na maswali hata baadae unaweza kuigawa hiyo brand kwa mwingine
sasa hivi cocacola wamebadilisha nembo wanatumia nyingine inatofauti kidogo na
ile ya mwanzo. Tayari kwa namna moja au nyingine umeshaiua brand yako na
umetengeneza tangazo la cocacola bila kujua.
- Inatakiwa
iwasilishe uhalisia wa biashara
,bidhaa au huduma
Nembo yako haitakiwi
kuwa nembo tu kama nembo,kwa vile nimesema hapo juu inatakiwa iwe ya kipekee
sijamaanisha basi utengeneze nembo ambayo haina hata kiwango wala haina maana
kwenye biashara yako inatakiwa nembo yako iwe na maana ndani yake ambayo maana
hiyo inapatikana ndani ya nembo au jina la brand hii inasaidia kutokumpoteza
mtu kutoka katika soko ulilopo mfano unahusika na usafirishaji sio lazima kenye
nembo yako kuwe na magari, ndege au meli ilikuonyesha kwamba unahusika na
usafirishaji unaweza kutengeneza nembo yako ikawa ni duara la dunia na alama ya
mshale juu unaoonyesha kuzunguka dunia tayari utakuwa umetoa zile alama halisi
kama gari na vyombo vya moto kwa kuweka alama ya mshale tu. Hivyo hakikisha
nembo yako inawasilisha unachokifanya lakini sio lazima iwe kwa picha ya moja kwa moja.
- Iwe na uwezo
wa kuonekana kwa wateja unaowategemea
Nembo sio alama tu
unayoitengeneza kukutambulisha tu katika soko inatakiwa pia iwe na mawasiliano
na mteja mtarajiwa iwe na uwezo wa kuonekana kwa wateja unaowategemea, mfano
kwa mteja ambae anampango wa kusafiri nje ya nchi anapoona alama ya dunia na mshale
katika logo yako na jina la kampuni ni comfort Transportation Company tayari
kichwani mwake anahisi hili kampuni ni la usafirishaji sio ndani ya nchi tu
hata nje ya nchi , hapo tayari kunakuwa na mawasiliano ya alama na hisia kati
ya nembo na mteja wako bila ya wewe mwenyewe kuwepo. Nembo yako hakikisha
inatosha kwenye macho yote mawili.
- Iwe na uwezo
wa kusimama na kujiimarisha muda hadi muda ( isipitwe na wakati)
Nembo yako haitakiwi
kuwa ya muda mfupi au ambayo inapitwa na muda unatakiwa kuwa na nembo ambayo
inauwezo wa kujisimamia muda wote na inauwezo wa kukaa kwenye soko muda wote
bila kupitwa na wakati mfano nembo ya brand ya maji ya Kilimanjaro ni nembo ambayo
inaonyesha mlima, japo ni brand ya maji lakini imetumia brand nyingine (mlima)
kujiongezea wateja na nembo yake haiwezi kupitwa na wakati hata kama mlima
utapunguza theruji na kupungua urefu bado nembo itaendelea kusimama vile vile
na haitapitwa na wakati , unatakiwa na wewe nembo yako pia iwe ya namna hiyo
isiwe ile ambayo inapitwa na muda .
- Iwe na uwezo
wa kutumika na kuoneka kwenye kila nyanja ya mawasiliano
Katika ulimwengu wa
utandawazi nembo yako inatakiwa iwe na uwezo wa kuonekana kwenye kila nyanja ya mawasiliano isiwe logo
ambayo ukiweeka sehemu fulani haiwezi kuaksi sehemu ilipo na mazingira yake
logo ambayo ukiiweka sehemu inapoteza muonekano wake wa asili, hiyo sio aina ya
logo unayotakiwa kuwa nayo au kuitumia kukutambulisha logo yako inatakiwa iwe
na uwezo wa kuonekana vizuri kwenye kila nyanja za mawasiliano.
Asante kwa kutuelimisha na elimu yako je ntajuaje kama nembo imekidhi hayo mahitaji ilhali sina uzoefu na grafiti
ReplyDeleteunapochagua sehemu ya kufanyia kazi lazima sasa ifikie hatua ya kuuliza uwezo na kazi zilizopita uwezo wa mtu huonekana katika kazi alizozifanya angalia kama kazi zilizopita zimekidhi haja ya maelezo ya hapo juu kama hazijakidhi mdadisi anauelewa gani na anachokifanya na kinaumuhimu gani kwa biashara yako akijibu kwa nafsi yake huyo sio wa kumpa kazi yako, logo unayotengenezewa wewe inatakiwa iwe kwa mawazo ya biashara yako aiangalie biashara yako sio kuangalia uwezo wake wa kuifanya kazi
ReplyDelete