Majibu ya Maswali 12 yahusuyo Branding

Kabla ya kuingia moja kwa moja katika somo la branding nimeonelea nitoe kwanza uzi wenye maswali na majibu kuhusu branding ili hata kwa yule ambae haijui na anahayo maswali ya msingi anaweza kuelewa na kupata picha ya kitu ambacho ninataka kuanza kukitolea ufafanuzi. Branding inahitajika kwa kila biashara na kila kitu kwa sababu hata wewe pia ni brand.

chini ni maswali na majibu kuhusu Branding

  1. Brand ni nini?

Ans: Brand kwa maana moja tunaweza kusema ni muonekano wa biashara yako, branding ni muonekano wako kuhusu biashara yako  na jinsi gani biashara yako inajitofautisha na washindani wenzako,


  1. Kazi za Brand.

Brand  hutambulisha muonekano ,ubora  wa kuaminika kwa watu, huku bidhaa za generic (kawaida)  hazijulikani  na haziaminiki ,hata hivyo brand ni ghali na inahitaji mipango ya muda mrefu

Brand hutofautisha bidhaa na hufanya bidhaa kutambulika mapema

Brand inaruhusu mtumiaji kutengeneza maamuzi na matumizi ya bidhaa

Brand hutengeneza thamani halisi kwenye macho ya washirika wa kibiashara na hupenyeza thamani ndani ya macho ya mtumiaji

Branding hutengeneza trademark ambayo huongeza thamani ya bidhaa.


  1. Kwanini ufanye brand

Unafanya brand kwa sababu unataka kutambulika na kuongeza mauzo , pia ni kutaka kujitofautisha na washindani wako

  1. Faida gani unayoipata ukibrand

Brand hukutambulisha,Brand hukutofautisha, brand hutengeneza thamani, Brand hukutengenezea trademark

  1. Hasara za kutokubrand

Hautajulikana kwenye soko,mauzo yako hayataongezeka,hautapata nafasi kwnye  ushindani

  1. Mifano ya Brand zilizofanikiwa

    1. Steps entertainment (usambazaji filamu za kitanzania)
    1. Msama promotion (matamasha- dini)
    1. Cocacola(Vinywaji)

                7. Mifano Brand zilizofeli

  1. General tyre
  1. TOL
  1. Tanganyika peackers
  1. NICO

                    8. Brand inasimamiwa na vitu gani?

    1. Nembo
    1. Brand
    1. Utambulisho
    1. kutokubadilika

                 9. Mgawanyiko wa Brand

    1. Brand ya mtu
    1. Brand ya Kampuni/mfumo
    1. Brand ya Bidhaa
    1. Brand ya Alama

 10. Nianze  kufanya nini?

Tengeneza Alama , halafu jibrand uje utengeneze mfumo then bidhaa

          11. Tofauti kati ya kampuni na Brand

Kampuni ni jina la wamiliki wa Brand
Na Brand ni  ahadi unayotaka kuiweka kwa wateja wako, ( ahadi ya mmiliki kwa mteja)
Kutafuta Masoko - ni kujenga brand kwenye akili ya mteja unaemtegemea

          12. Tofauti kati ya elimu ya ujasiriamali na branding

Elimu ya ujasiriamali- ni elimu inayotolewa kwa ajili ya kukutengenezea njia za kujiajiri na kujiongezea mapato.

Elimu ya Branding - Ni elimu ya kujua jinsi ya kuongeza mapato na kujulikana kwenye kipengele chako  cha ushindani

Comments

Popular posts from this blog

Baadhi ya vitu vinavyosababisha biashara nyingi kufungwa.

Umuhimu na maana ya Logo( Nembo) katika biashara yako.

Aina za malengo na mipango