Maana ya Branding katika Biashara/ujasiriamali wako




Brand ni rasilimali inayotokana na ahadi ambayo inaunganishwa na bidhaa kwa wateja wake.Au brand ni alama inayotambulisha nafasi yako kwenye soko lako la ushindani.

Shughuli ya brand inatakiwa iwe imedizainiwa na kuandaliwa maalum  kwa ajili ya biashara yako kukutofautisha na wapinzani wako kibiashara. Hata kama wapinzani wote wanamuonekano
Mzuri au kukushinda wewe .


1. Brand yenye mafanikio huzingatia sanaumoja,Inapojitambulisha haijitambulishi kwa vitu vingi

Mfano:1.  Kampuni ya Cocacola wanabidhaa nyingi lakini ukiona matangazo yao wamejikita sana kwenye kuitangaza cocacola yenyewe. ikiwa inamaanisha japo wanabidhaa nyingi bidhaa zote zinajitengenezea au zinatengenezewa brand yake yenyewe.


2.     Kuna tofauti kati ya mauzo na kubrand.
Rolex Orijino

Rolex feki
Mfano: unaweza kuuza saa ya Rolex dola 100? Ni kweli inawezekana kuuzwa kwa bei hiyo
   na zikauzwa nyingi lakini nini kitatokea baada ya muda mrefu kwenye brand ya Rolex.
zitatoka rolex za bei ya chini ambazo zinauwezo wa kuua kabisa soko la rolex za mwanzo
  ( Hii inamaanisha brand iliyofanikiwa huwa haionekani kwa kila mtu)

3.     Kutafuta masoko ni kujenga brand kwenye ubongo wa unaemtegemea.

4.     Masoko ni malengo makubwa ya kampuni,ndio maana asilimia kubwa ya watu wanaofanya kazi
Kwenye makampuni  lazima huwa wanakuwa wameunganishwa na sekta ya masoko

5.     Sasa hivi dunia ya biashara ipo kwenye utaratibu wa kuhama kutoka KUUZA kwenda KUNUNUA.
Na kuhama huku kumechangiwa na kusababishwa na kubrand.(kujenga alama)

Watu wa masoko wanamaana zote za jina la kampuni,majina yalivyogawanyika,majina ya brands na
Majina ya mamodels ( wanaoigwa) hata brand ndogo ndogo,brand kubwa ,brand rafiki nakadhalika
Lakini ukiangalia ndani ya kichwa cha mteja unaemtarajia, hayo yote yanapotea  hebu fikiria mteja
Anaongea na rafiki yake " hivi unaifikiriaje kuhusu hii Basic  branding , project mpya ya Legacy impresion

Brand haina kitu kingine tofauti ila ni neno lililoko ndani ya kichwa na mawazo lakini ni neno maalum
La aina yake. Jina la brand ni jina la kawaida kama mengine linalotamkwa kwa herufi kubwa na kila
Jina halisi ni brand  haijalishi linamilikiwa na nani mtu binafsi ,kampuni au jamii.
 
Mfano: Kilimanjaro ni jina la brand inayoongoza kwa kuuza maji ya kunywa, lakini pia ni brand jina la
Mlima na mkoa pia.

Kila jina halisi ni brand, hata wewe pia ni brand na kama unataka kufanikiwa kikweli kweli kwenye
Maisha yako unatakiwa kujichukulia wewe mwenyewe kama brand  na ufuate sheria ya kujibrand.

Nguvu za kubrand zinategemea uwezo wa kuchukua na kutumia tabia.

Mfano: mteja anaeingia shoprite kuchukua mkate na maziwa kawaida  huishia kuchukua bidha kutoka brand mbili tofauti, japo inaweza kuwa au haipo kuchagua brand ndani ya kichwa chake.ni  maziwa na mkate vyote ni bidhaa zisizo kuwa na tofauti sana.Lakini mteja huyo huyo akinunua katoni ya bia na sigara nafasi ya mnunuzi kutafuta brand anayoitaka ni kubwa. Maana yake ni kwamba mkate na maziwa ziko katika kundi la kununua bidhaa lakini bia na sigara ziko katika kundi la kununua brand.

          LAKINI UNAWEZA KUBRAND KWENYE KILA JINA HALISI


Ungana nami zaidi kupitia ukurasa wangu wa facebook : Elisha

 Chuma ("like" ukurasa huu na utapata habari zote na machapisho

 mara tuu ninapotoa.) Asante

Comments

Popular posts from this blog

Baadhi ya vitu vinavyosababisha biashara nyingi kufungwa.

Umuhimu na maana ya Logo( Nembo) katika biashara yako.

Aina za malengo na mipango