Maana ya Branding kwa mfanyabiashara na Mjasiriamali

 
                                         Maana ya branding kwa mfanyabiashara

Branding ni muonekano wa biashara yako kwa mteja unaemtarajia  kwa maana hiyo brand
Inahusika na inanafasi kubwa katika ukuzaji wa biashara yako na  maendeleo yake kila  jina ni
Brand lakini sio kila brand ni jina hivyo ili jina liwe brand linahitaji  vitu fulani fulani ili kuwa hivyo

Mfano: Naseeb Abdul ni jina lakini Diamond ni brand.

Ikiwa inamaana ya kwamba ili uwe na kitu au Uonekane katika kipengele au sehemu yako ya ushindani ni lazima uwe na brand na sio jina.Ukiwa kama mfanyabiashara ambaye unafanya biashara sio kwa majaribio brand ni lazima katika  biashara yako , Brand inatakiwa kuanza kutengenezwa tangia mwanzo wa biashara  ili kuipa nguvu ya kuwepo sokoni kwa muda mrefu na pia kutengeneza kitu ndani ya vichwa vya wateja wako na wateja unao wategemea

Mfano: Serikali ilipoamua kuhama kutoka analojia kwenda dijitali  kampuni nyingi zilikuwa 
                hazijajipanga kuwa mawakala wa utoaji chaneli hizo kampuni zilizokuwepo ambazo zilikuwa 
               zinasikia ni startimes na multchoice(dstv) lakini ghafla yakaanza kutokea matangazo ya
               king;amuzi kipya cha digitek, matangazo hayo yalikaa kwa muda bila ya kukiona king'amuzi 
               hicho wala ofisi zao ila tu kwenye televisheni,watu walipata hamu ya kuwa nacho hata kabla
               Ofisi zake hazijulikani na kilivyokuja kutoka watu walivinunua vingi kwa bei ya juu hii ni  
               kutokana tu na matangazo ambayo yalitoka hata kabla ya king'amuzi chenyewe kutoka.

Maana ya mfano huu ni kwamba kampuni ilianza Kutengeneza brand ya bidhaa yao hata kabla bidhaa haijatoka kwa nia ya kipindi cha kuitoa bidhaa kitakapofika Bidhaa ipate nafasi katika soko. Hivyo kutengeneza brand tangia mwanzo wa biashara kuna faida kubwa

Ikiwa inamaanisha  ili biashara yako ikubalike au ipate nafasi nzuri ya kuonekana
Kwa mteja wako ni lazima uwe umeibrand, brand iko kwenye kila kitu hivyo unaweza
Kufanya brand bila kujua kama unafanya brand .

Hivyo ukiwa kama mfanyabiashara,mjasiriamali au mtu yeyote unaetegemea kuleta au kuingiza kitu chochote
Chenye ushindani tengeneza brand ya bidhaa yako unayoileta .

Unaweza kupata maelezo zaidi kuhusu branding kwenye matoleo yangu ya nyuma pia nitaendelea kuwafafanulia
Brand hatua kwa hatua kadri siku zinavyoenda usikose kupitia kwani yanamanufaa sana kwako na kwa kizazi chako utakachokuja kukifundisha.

Comments

Popular posts from this blog

Baadhi ya vitu vinavyosababisha biashara nyingi kufungwa.

Umuhimu na maana ya Logo( Nembo) katika biashara yako.

Aina za malengo na mipango