vitu vya kutambua baada ya kuwa mfanyabiashara au mjasiriamali
biashara au ujasiriamali ni ndoto za watu wengi lakini asilimia kubwa husahau vikwazo na vizingiti ambavyo hutokea kabla na baada ya kuwa mjasiriamali au mfanyabiashara toleo lililopita nilielezea vitu unavyotakiwa kufanya kabla ya kuwa mjasiriamali, leo nitaelezea vitu unavyotakiwa kuvifanya baada ya kuwa mjasiriamali .
kuna vitu na mambo mengi ambayo unatakiwa kuyafata ili ufanikiwe katika kila hatua ya biashara au ujasiriamali wako baadhi ya vitu hivyo ni pamoja na
2. Muonekano wako unaathiri
biashara yako
3.Maneno yako ndio biashara
yako
5. Usiwe na tamaa
Ukiwa mfanyabiashara au mjasiriamali unatakiwa usiwe mtu wa tamaa, mtu ambae ukitamanishwa kitu mara moja umeshakitamani na unataka kuwa nacho hiyo ni mbaya kwa sababu ukiwa kwenye biashara utakutana na wafanyabiashara wengi na wa aina tofauti kuna wengine watakushawishi ujiunge na biashara zao, kuna wengine watakupa mawazo ya biashara nyingine inaweza kuwa ni kwa nia nzuri au mbaya lakini kitu kikubwa na cha msingi ni usiwe na tamaa simamia biashara yako hadi uhakikishe imefikia hatua uliyokuwa unaiota hapo ndio unaweza kuanza kufata ndoto za watu wengine .
6.Fanya biashara yako kwa
mipango
7. Brand biashara yako kwa hatua
uliyopo.
kuna vitu na mambo mengi ambayo unatakiwa kuyafata ili ufanikiwe katika kila hatua ya biashara au ujasiriamali wako baadhi ya vitu hivyo ni pamoja na
Baada
ya kuwa mjasiriamali au mfanyabiashara
1. Biashara ni ushindani, na
nafasi ya makosa
Moja
kati ya vitu ambavyo unatakiwa kutambua ni biashara ni ushindani ili biashara
Iendelee
lazima ipate ushindani wa kutosha ndipo biashara itakuwa biashara ila kama
Hakuna
ushindani hautakuwa unafanya biashara bali unatoa huduma,mfano kwa kampuni kama
Tanesco
wao hawafanyi biashara wanatoa huduma kwa sababu hawana mshindani wa moja moja
, katika Biashara
kuna aina tatu za washindani kuna washindani wa moja kwa moja ( hawa ni wale
ambao wanafanya biashara ka ma ya kwako), wasio wa moja kwa moja ( hawa ni wale
ambao wanafanya biashara mbadala wa biashara yako) na wa tatu ni dhahania (
hawa ni wale ambao hawajaanza kutoa huduma au kufanya biashara lakini wana wazo
la kufanya biashara kama yako), kwa Tanesko wao hawana mshindani wa moja kwa moja
ila wana washindani wasio wa moja kwa moja kama wauza jenereta na umeme wa jua.
Hivyo katika biashara ushindani ni kitu muhimu ili uendelee unapokuwa
mfanyabiashara au mjasiriamali lazima
utegemee ushindani na kila siku angalia vitu viwili kwa makini katika biashara
yako wateja wako pamoja na washindani
wako .
Kitu
kingine cha kuongezea hapo ni pia ukiwa mfanyabiashara unatakiwa utambue
biashara ni nafasi ya makosa, mshindani wako muda wote anaangalia unamapungufu
gani ili atumie mapungufu yako
kujiongezea wateja hivyo unatakiwa kuwa makini kuangalia mapungufu ya
washindani wako na pia kuangalia maamuzi
yako,mbinu unazotumia kuongeza wateja na aina ya ujumbe unaoufikisha kwa
jamii.asilimia kubwa ya washindani hutumia vitu hivyo kuona mapungufu yako.
Ukiwa
kama mfanyabiashara au mjasiriamali muonekano wako unanafasi kubwa sana katika biashara yako na muonekano huu
unajumulisha ,mavazi, matendo na uwezo
wako wa kufikiri mara nyingi akija mtu
ambae anahitaji kukudadisi na kujua unafanye biashara yako ni lazima atakuuliza
kuhusu matatizo mnayoyapata na njia mnazotumia kuyatatua hii yote ni kuangalia
ni kiasi gani unauwezo wa kukabiliana na matatizo na je ni mtu wa aina gani
anaeongea nae , hivyo mara zote angalia sana muonekano wako kuanzia kwenye
familia yako hadi kwenye jamii yako ni
jambo la kawaida kusikia " ooh fulani ameanzisha biashara fulani "
halafu jibu linatoka " mlevi huyo haiwezi kudumu " hii inamaanisha
alieanzisha hiyo biashara muonekano wake na jamii inamchukulia kama mlevi na tayari muonekano huo unaunganishwa moja moja
kwenye biashara yake japo biashara sio yeye ila muonekano umemtengenezea.
Hakikisha muonekano wako unashabihiana na biashara yako na nafasi uliyonayo
katika jamii.
Kitu
kingine kinachosimamia biashara ni kauli, au maneno yako mwenyewe, ukiwa kama
mfanyabiashara unatakiwa mdomo wako uwe na nidhamu na uwezo wa kutamka yaliyo
ya staha na pia unatakiwa uzijue lugha za biashara ili kutofautisha majibu
unayoyatoa nyumbani sio sawa na unapokutana na mteja ,mfanyabiashara au
mjasiriamali mwenzako .
4.Sheria za pesa
Ukiwa
kama mfanyabiashara au mjasiriamali unatakiwa uzijue na sheria za pesa pia ,
sheria kuu ya pesa ni matumizi hivyo pesa sio ya kutunzwa ili ikuzalishie
nyingine pesa ni ya kutumiwa ili ikuzalishie nyingine, watu wengi huwa
wanaamini mtu mwenye pesa nyingi ni yule ambaye akaunti yake inasoma fedha
nyingi kwa nji za wenzetu na watu waliondelea sawa lakini kwa wafanyabiashara
wadogo na wafanyakazi ni uongo, mfano : utakuta mtu ametunza mshahara wake
kachanganya na fedha zake za pembeni akihisi ni hela ya kuweza kuongea na mtu
na ukamwambia basi utasikia sasa hivi nnahela
kama millioni 10,20,50,90. Lakini ile fedha ukiingalia kwa umakini sio
ya kwake mimi ninaamini kwamba lile karatasi au sarafu unayoishika huwa ni
karatasi na sarafu za kuwakilisha thamani tu na ukiwa nalo sio la kwako mfano:
umelipwa mshahara millioni 10 ukitoka tu kuwepa tayari inakuwa imeisha hata
kabla haujaitoa mikononi mwako sababu
hiyo pesa tayari inamahitaji yake. Kuna
siri moja iko hivi wewe unapofanya kazi ili ulipwe unakuwa unaifanyia
mipango hela ambayo atakupa bosi wako lakini pia kuna mtu mwingine ambae pia
anakusubiri ukishaichukua hiyo pesa umpelekee
wewe ni bosi wake na yeye pia kuna mwingine ambae akishaichukua hiyo
fedha ni lazima amplekee ili aishi huo ndio mzunguko na sheria ya pesa.maana au
nia ya kukuambia hivyo ni ukiwa mfanyabiashara au mjasiria mali ifanye hela
yako izunguke isiwe ya kukaa na kuhesabiwa tu.
Ukiwa mfanyabiashara au mjasiriamali unatakiwa usiwe mtu wa tamaa, mtu ambae ukitamanishwa kitu mara moja umeshakitamani na unataka kuwa nacho hiyo ni mbaya kwa sababu ukiwa kwenye biashara utakutana na wafanyabiashara wengi na wa aina tofauti kuna wengine watakushawishi ujiunge na biashara zao, kuna wengine watakupa mawazo ya biashara nyingine inaweza kuwa ni kwa nia nzuri au mbaya lakini kitu kikubwa na cha msingi ni usiwe na tamaa simamia biashara yako hadi uhakikishe imefikia hatua uliyokuwa unaiota hapo ndio unaweza kuanza kufata ndoto za watu wengine .
Usifanye
biashara kwa kupelekwa pelekwa panga mipango yako kabla ya kuanza kitu chochote
na katika hiyo mipango usisahau kuweka plan b, ukiwa unapanga biashara yako kwa
mipango itakupunguzia kuyumba kuyumba na pia kuyaona mafanikio au kushindwa kwa
biashara mapema.
Brand
ina maana nyingi na ni kubwa lakini kwa ufupi ni Brand ni muonekano wa bidhaa
yako na ahadi uliyoweka kwa mteja unayemtarajia ,lakini brand pia imegawanyika
katika aina kuu nne ambazo ni alama , mfumo,mtu
na bidhaa ambavyo vyote hivyo hufanya kazi pamoja ili upate mafanikio na majibu unayoyataka katika
biashara ( nitaelezea siku nyingine kuhusu branding) hivyo kwa kuwa brand ndio
msingi wa biashara na kuifanya brand kubwa ni gharama unatakiwa uifanyie brand
yako kwa kila hatua unayokuwepo mfano: unaweza kuwa na kampuni ya kuuza
kutengeneza unga lakini kwa kuanza hauna fedha ya kuibrand biashara unaweza
kuanza kwa kufanya brand ya alama kwa maana ya muonekano wako kwa wateja wako,
ukatengeneza nembo pamoja na vitu vichache vya kutumika ofisini baada ya hapo
ukachapisha na mifuko ya kuwekea unga tayari hapo unafanya brand ya bidhaa yako
ukimaliza hapo utakuwa unauza hadi ukiona unahama sehemu ya kwanza unaweza sasa
kutengeneza mfumo kwa wafanyakazi wako kuwavalisha sare na baade pia kuanza
sasa na kujitangaza hata kwenye mabango ya barabaani na kwenye runinga.
This comment has been removed by the author.
ReplyDeleteNi kweli Mr. Silas ili uwe mjasiriamali unatakiwa kuwa jasili sana sababu kuna mambo mengi ya kutataua na vizingiti vya kupita lakini kuwa jasiri peke yake hakutoshi kukufanya uwe mjasiriamali kuna vitu ambavyo ni muhimu kuvitambua kabla haujaanza ujasiriamali ili vikuongoze katika ujasiri wako na kukamilisha ndoto yako
ReplyDelete