Ukweli kuhusu ujasiriamali


Nimeshaandika sana kuhusiana na ujasiriamali japo sijafikia sehemu ambayo inatakiwa lakini inatakiwa tufikie hatua tuache kudanganyana kuwa mjasiriamali sio suala dogo  lakini watu wamefanya kama vile ni kitu ambacho kila mtu anaweza kukifanya, ujasiriamali sasa umekuwa ni wimbo kila mtu ni mjasiriamali hata muuza vitumbua nae ni mjasiriamali tunapoteza vijana wengi kwa wadanganya kuhusiana na ujasiriamali , ukweli ujasiriamali ni mgumu na tena sio mgumu kidogo ni mgumu sana.

Ukianza kiuangalia nadharia ya ujasiriamali  ni mtu mwenye ujasiri na nguvu kwenye mali lakini tofauti na ambavyo tunauangalia kwa upande mwingine ambavyo ndivyo asilimia kubwa wanafahamu kwamba ujasiriamali ni uwezo wa kufanya au kumiliki biashara yako , huo ni uongo tena mkubwa, tunakopi vitu kutoka nchi zilizoendelea halafu tunatafsiri vibaya , ukiangalia watu wanaoitwa wajasiriamali kwa nchi za nje ni tofauti kabisa na wanaoitwa wajasiriamali wa huku, na kitu kibaya zaidi ni kwamba tunakopi mifano ya kuvutia (Inspiration) kutoka kwao lakini hatufanyi kama wao,taifa tunalolitengeneza  sio tunaloliombea , tunajitahidi kila siku kuwa tuna washawishi vijana wetu kufanya ujasiriamali wa kujiajiri mwenyewe , hata hapo pia haiwezekani hakuna mjasiriamali aliefanikiwa kwa kufanya ya kwake  peke yake wote ambao ndio mifano yako ya mvuto fuatilia ni lazima aliajiriwa kwanza au alianza kwenye sehemu ya mwingine halafu  baadae ndio anaanza kuja kufanya sehemu yake , hivyo usije ukadanganywa  eti ukitaka kufanikiwa inabidi ujiajiri mwenyewe kwanza  ni lazima uajiriwe kwanza au upate ujuzi wa hiyo kazi ndio uanze kujiajiri, na ujuzi unaopewa katika ngazi za elimu zetu ni wa kusaidia kompyuta kukamilisha kazi yake, hivyo kuajiriwa ni lazima kabla ya kuanza kutembelea ndoto yako, hasa kwa nchi ambazo zinaendelea kwa sababu uwezo wa kutengeneza na kuvumbua umedidimizwa na vitabu vya wavumbuzi wengine wa zamani.

Ujasiriamali ni kitu ambacho unatakiwa  kutulia sio kukurupuka nacho ni lazima ujifunze kuwa na subira na usifanye ujasiriamali kama mpango wako ni  kupata fedha peke yake kwa sababu unapokuwa  mjasiriamali ni lazima ufanye biashara kwa matokeo ya baadae mjasiriamali hafanyikitu kwa ajili  ya faida au matokeo ya muda mfupi ndio maana asilimia kubwa ya mifano ya watu tunaowaona kama mifano katika maisha ya ujasiriamali hawakuanzia kwenye mafanikio ila wameanzia kwenye hali ya kawaida sana na ya chini lakini mafanikio yao yamekuja baada ya muda mrefu tofauti na sisi ambao mawazo ya ujasiriamali tunapewa halafu bado tunataka tufanikiwe ndani ya kipindi kifupi, wote waliofanikiwa na kuwa wajasiriamali mifano walikuwa wanaishia ndoto zao kuna ambao kutokana na kuyaamini mawazo yao na kuyakubali kwa kiasi kikubwa iliwagharimu hata elimu zao kuna walioacha masomo sababu ya kufatilia ndoto zao,wapo walioacha kazi na hata familia lakini tofauti na kwetu unakuta  mtu hajajiandaa hata kuwa na hiyo ndoto unatembea na ndoto mbili au ndoto zaidi ya nne na bado hata haujakamilisha moja unapewa ndoto nyingine ili ukamilishe ndoto yako mpya, ukweli ni kwamba hapo utakuwa unatumikia ndoto ya mtu mwingine huku unazika za kwako na huwezi kufanikiwa pia ukiwa na ndoto zaidi ya moja ifikie hatua watu wajitambue  ndoto ni moja na hiyo ndio itakayo kupa mafanikio yako , tunatengeneza taifa ambalo litakuja kuwa zaidi ya tegemezi sababu baada ya muda  hao tunaowaita wajasiriamali hawatakuwa na uwezo wa kusimamia tena biashara zao na wataanza kutafuta misaada watakaokuwa na pesa kwa kipindi hicho watakuwa ni wale waliokomaofisini na wafanyabiashara hivyo pesa itakuwa mikononi mwa watu wachache na hao watawaburuza hao wanaojiita wajasiriamali.

Kuna mengi ya kuamua kabla ya kuwa mjasiriamali tusikurupuke na kuanza kujiita tu wajasiriamali jiulize kwa maelezo hayo hapo juu wewe ni mjasiriamali au mfanyabiashara , na gundua ndoto yako mapema na uifanyie kazi sio kukaa pembeni na kusubiri elimu ikuamulie kazi yako, soma unachokitaka sio fedha inachokitaka unatakiwa kujua kuwa fedha ni matokeo ya huduma hivyo jifunze huduma ambayo itakupa furaha na faraja hata bila ya kupata pesa kama tokeo la mwisho ujasiriamali sio kitu kidogo yafaa kuelewa maana kwanza na sio kufanya kwa mkumbo unaweza kupoteza muda na fedha zako bure.tuache kutengeneza tafsiri nyepesi ya maneno magumu.

Fuatilia masomo ujasiriamali na biashara kupitia semina ya MAFANIKIO maelezo zaidi yako kwenye matoleo ya nyuma na  ukurasa wa matangazo.


Comments

Popular posts from this blog

Baadhi ya vitu vinavyosababisha biashara nyingi kufungwa.

Umuhimu na maana ya Logo( Nembo) katika biashara yako.

Aina za malengo na mipango