Vitu 10 (Kumi) vitakavyofanya biashara yako ifanikiwe
Bishara yako haiwezi kujiendesha yenyewe bial kuwa na vitu vinavyoisimamia leo nimekuletea vitu 10 vitakavyoifanya biashara yako ifanikiwe, ni vitu ambavyo tunaviona ni vidogo na vipo katika maisha yetu ya kila siku hivyo tunavifanyia mazoea lakini sasa
8. Sifia na kubali kukosolewa.
1. Ipende biashara yako.
Biashara yako ni
maisha yako ndio mfereji wa kipato chako hivyo inatakiwa ipendwe na
kuthaminiwa,unapoweka upendo wa kutosha kwenye biashara yako lazima mafanikio
yatakuja yatakayokuja, fanya biashara kwa upendo na moyo wa kujituma.usifanye
biashara yako kama ya jirani yako ipende na ithamini itakupenda na itakulipa.
2. Jenga uamninifu.
Katika biashara kitu
cha muhimu kuliko yote ni uaminifu sababu mteja anapokuja kununua au kupokea
huduma kutoka kwako ni kutokana na uaminifu kwako na kuamini huduma yako
hivyo fanya kazi kwa uaminifu sikuzote
kwa mafanikio na maendeleo ya biashara yako.Uaminifu wako ndio mafanikio yako
fanya kila kitu kwa uamnifu .
3. Usibadilike badilike.
Moja kati ya vitu
vinavyoondoa uaminifu na muonekano wako mbele ya wateja wako ni kubadilika
badilika leo unafanya biashara hii kesho biashara ile unaua maendeleo ya biashara
yako,kutokubadilika ni siri ya mafanikio ya biashara nyingi, watu wengi huwa
wanachanganya kati ya kutengeneza sub-brand na kubadili biashara. Mfano
watengenezaji wa bia ya Castle lager walipoleta Castle lite sio kwamba
walibadilisha biashara bali walileta sub brand( brand saidizi) ni tofauti iwapo
Castle lager wangeamua kuleta kinywaji kingine chenye jina tofauti na Castle
huku watengenezaji wakiwa ni wao wenyewe hapo ingekuwa wamebadilisha brand
(muonekano,picha ya biashara),usibadilike badilike kwa kufata upepo wa pesa toa
huduma au bidhaa pesa iwe ni matokeo ya huduma au bidhaa.
4. Usiruhusu uoga /kushindwa kukakurudisha nyuma
Biashara ni
mashindano na katika mashindano nia kuu ni kushinda hata kama mpinzani wako
unamfahamu anauwezo kiasi gani matarajio ni kushinda, pia hata katika biashara
ni hivyo hivyo nia kuu ni mafanikio na biashara kukua hata utakutana na vikwazo
kiasi gani hautakiwi kushindwa ,pesa ni mchezo wa kunyang'anyana wewe unapokuwa
nayo ni mali ya mwingine na mwingine anapokuwa nayo ni mali yako, iwapo utakuwa
muoga au ukikubali kushindwa utakuwa
unapokea tu mali ya wengine bila wewe kuchukua ya kwako.Usikubali kurudishwa
nyuma changamoto ndio biashara. Uoga wako utakupotezea mafaniko yako iwapo utauruhusu
5. Fanya maamuzi kwa kuendana muda.
Hapa pia kuna tatizo
kubwa kwa upande wa hapa kwetu maamuzi yetu hayaendani na muda ila yanaendana
na mawazo yetu, muda nnausemea hapa sio ule wa dakika ama saa ila muda kwa
maana ya maamuzi ya kibiashara kulingana na hali ya soko, asilimia kubwa ya
wafanyabiashara wanandoto za kufanikiwa kuwa kama watu wanaowatamani kutokea
nje ya nchi na wengine ndani ya nchi pamoja na kuwa hivyo lakini tatizo
linakuwa unatamani kuwa kama yeye lakini haufanyi kama yeye.hapo haitawezekana
itakuwa sawa na serikali ilipoamua kupunguza wimbi la ajira kwa vijana kwa
kuruhusu ujasiliamali wa vitu vidogo vidogo
lakini baada ya muda ikangundua dunia inatumia barcode na hawapati kodi
sasa wameamua kuanzisha utaratibu wa ili bidhaa yako iwe sokoni ni lazima ipitie TBS na TPDF kwa ajili ya
kuhakikishwa kwanza hii ni kufanya maamuzi ya mwanzo bila kuendana na wakati
Barcode na shirika la viwango yapo toka zamani na matumizi yake yanajulikana
tangu zamani lakini sasa madhara yanakuja kwa mjasiriamali mdogo ambae hawezi
tena kufatilia na kufuata taratibu zote mwisho ni kwamba unamrudisha alikokuwa
mwanzo. Tumia muda na maamuzi yako kwa kuendana na soko lako na matokeo ya
baadae usifanye kwa ajili ya leo na kesho kuna kesho kutwa ambayo hauwezi
kuirudisha.
6. Kumbuka wewe ni mhimili mkubwa katika biashara.
Japo biashara yako
sio ewe lakini ukweli ni kwamba biashara ni wewe mwenyewe unatakiwa kutambua
kuwa
inakutegemea wewe mwenyewe ili iweze kukuletea faida ,muonekano wako,
majibu yako, maamuzi yako, mavazi yako yanamatokeo ya moja kwa moja kwa mteja
na biashara yako hivyo unatakiwa ujitambue na uione nafasi yako katika biashara
yako .
mafanikio au kufeli kwa biashara ni kutokana na maamuzi yako wewe ndio
mhimili wake , Biashara yako7. Simamia vizuri wivu wako.
Katika biashara napo
kunatakiwa wivu na hakuna mtu asiekuwa na wivu lakini hapa unachokumbushwa tu
ni kuusimamia vizuri wivu wako, wivu wa biashara ni ule wivu ambao unamuona
mfanyabiashara au mjasiriamali mwenzako amepata mafanikio na wewe unapata wivu wa
hamu ya kuwa vile,lakini hiyo hamu unayoipata ndio inatakiwa iwe na kiasi
mfano; wewe unauza nafaka na mwenzako pia anauza nafaka mwenzako akaanza
kutafuta masoko akapata wateja wengi akaongeza mtaji wewe bila kugundua kiini
cha mafanikio na wewe ukachukua mtaji na faida vyote ukaviweka ili biashara
yako ilingane na biashara yake hapo utakuwa umepotea kwa sababu kesho na kesho
kutwa ukipata tatizo hautaweza kulimudu sababu malengo yako yamehamishwa na
sasa unakuwa mtumwa wa mafanikio ya mtu mwingine. Usimamie wivu wako uwe na
kiasi na ujifunze kufatilia mambo kwa undani.
Kuna watu ukiwakosoa
ni kama umetenda kosa la jinai , mara zote wao hujiona wanajua kila kitu na
wanaweza kufanya kila kitu lakini ukweli ni kwamba anaejiona anajua kila kitu
huyo ni mjinga, na mjinga akifeli hujiona anaweza sana kwa sabau hutengeneza njia za kujilinda
na kufeli kwake, hivyo ili biashara yako ifanikiwe kubali kusifia kuanzia
unaofanya nao kazi hadi washindani wako, biashara sio sehemu ya kusambaziana
chuki na uhasama wote ni binadamu na tuliumbwa na upendo hata kama ni mshindani
wako akifanikiwa msifie na wewe pia
kubali kukosolewa hauwezi ukafanya kila
kitu sawa sawa hata kama unakijua
asilimia 100, kuna aina nyingi mno za makosa ya kiufundi, binafsi, ya
mitambo n.k hivyo ukikosolewa ni njia mojawapo ya kupewa mbinu ya kufanikiwa
kwa sababu biashara ni mchezo wa kutumia makosa ya mwenzako.
9. Simamia kufanya kazi kwa bidii na umoja.
Siku zote katika
biashara yako himiza na simamia ufanyaji kazi kwa bidii na kwa umoja iwapo
ofisi ikifanya kazi kwa bidii na umoja mafanikio yake yataonekana mapema ila kama ufanyaji kazi utatawaliwa na chuki
pamoja na visasi hakutakuwa na mafanikio yanayotarajiwa, yafaa turudi
tulikotoka "utu kwanza pesa baadae" na umoja ni msingi wa mafanikio simamia hapo na
matokeo yake yatakuja hivi karibuni.
10. Kuwa na Imani.
Kila mtu anaimani na
kitu anachokiamini hivyo weka imani yako pia katika biashara yako hata kama
matokeo nafaka ni sawia
kesho unaamini kuuza magari ndio sawia hapo hautafanikiwa biashara ni ile ile
kila sehemu kuna changamoto zake amka sasa iamini biashara yako na ipe hadhi ya
imani yako utafanikiwa.
yake sio mazuri kwa kipindi kirefu angalia tatizo ni nini na iamini
ndio biashara itakayokupa mafanikio na kukufikisha katika ndoto zako usiifanye
kwa kujaribu fanya kwa nia na imani ya juu,usichanganye imani katika biashara
moja leo unaamini kuuza
Hivyo ndivyo vitu 10
vitakavyofanya biashara yako ifanikiwe na ikue hadi mahala unapopahitaji hakuna
miujiza katika biashara na hakuna mazingaombwe katika biashara ni kutambua yanayokufaa na kuyafanyia kazi kwa moyo na ari ya kutaka
kuyatimiza, mafanikio yako kwa kila mtu "umezaliwa ili ufanikiwe sio
ufeli" tumia mbinu hizo na utafanikiwa.
hakika Mungu alibariki kwa makala yako
ReplyDelete